>>AZAM YAINYUKA KAGERA, YABAKI KILELENI!
MATOKEO:
Jumapili Februari 2
Yanga 1 Mbeya City 0
Azam 4 Kagera Sugar 0
LEO, Jijini Dar es Salaama zilichezwa Mechi mbili za VPL, Ligi Kuu Vodacom, zikihusisha Timu 3 za juu na Azam FC kubaki kileleni baada kuinyuka Kagera Sugara Bao 4-0 huko Azam Complez, Chamazi na Yanga kuipa kipigo cha kwanza kwenye Ligi Mbeya City na kubaki Nafasi ya Pili.
SOMA ZAIDI:
YANGA 1 MBEYA CITY 0
Bao la Dakika ya 16 la Supastraika,
Mrisho Ngassa, liliwashushia Mbeya City kipigo cha kwanza kwenye Ligi na
kuifanya Yanga izidi kujichimbia Nafasi ya Pili ikiwa Pointi 1 nyuma ya
Azam FC.
Mbeya City, ambao walipigana kiume,
walipata pigo mara tu baada Kipindi cha Pili kuanza baada ya Mchezaji
wao Steven Mazanda kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
AZAMFC 4 KAGERA SUGAR 0
Huko Azam Complex, Chamazi kwenye Viunga
vya Jiji la Dar es Salamm, Wenyeji na Vinara wa VPL, Azam FC,
waliendelea kukaa kileleni baada kuinyuka Kager Sugar Bao 4-0.
Bao za Azam FC zilifungwa na Brian Umony, Bao mbili, na nyingine kupitia Jabir Aziz Stima na Kevin Friday.
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano Februari 5
Tanzania Prisons vs Coastal Union
(Uwanja wa Sokoine, Mbeya)
(Uwanja wa Sokoine, Mbeya)
Mgambo Shooting vs Ruvu Shooting
(Uwanja wa Mkwakwani, Tanga)
Rhino Rangers vs Oljoro JKT
(Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora)
JKT Ruvu vs Ashanti United
(Uwanja wa Azam Complex, Chamazi)
MSIMAMO:
NO
|
TEAMS
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
1
|
Azam FC |
16
|
10
|
6
|
0
|
29
|
10
|
19
|
36
|
2
|
Young Africans |
16
|
10
|
5
|
1
|
34
|
12
|
22
|
35
|
3
|
Mbeya City |
16
|
8
|
7
|
1
|
22
|
13
|
9
|
31
|
4
|
Simba SC |
15
|
8
|
6
|
1
|
31
|
13
|
18
|
30
|
5
|
Mtibwa Sugar |
15
|
5
|
6
|
4
|
19
|
18
|
1
|
21
|
6
|
Kagera Sugar |
16
|
5
|
6
|
5
|
15
|
15
|
0
|
21
|
7
|
Coastal Union |
15
|
3
|
9
|
3
|
11
|
8
|
3
|
18
|
8
|
Ruvu Shootings |
14
|
4
|
6
|
4
|
16
|
16
|
0
|
18
|
9
|
JKT Ruvu |
14
|
6
|
0
|
8
|
13
|
18
|
-5
|
18
|
10
|
Rhino Rangers |
15
|
2
|
5
|
8
|
9
|
18
|
-9
|
11
|
11
|
JKT Oljoro |
15
|
2
|
5
|
8
|
10
|
15
|
-5
|
11
|
12
|
Ashanti United |
15
|
2
|
4
|
9
|
13
|
28
|
-15
|
10
|
13
|
Tanzania Prisons |
13
|
1
|
6
|
6
|
6
|
16
|
-10
|
9
|
14
|
Mgambo JKT |
15
|
2
|
3
|
10
|
7
|
26
|
-19
|
9
|
TAARIFA TOKA TFF:
Release No. 016
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 2, 2014
TARIMBA KUONGOZA KAMATI YA NIDHAMU
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imefanya uteuzi wa wajumbe kuunda kamati
mbili za awali za haki, na kamati mbili za rufani za vyombo hivyo.
Rais wa zamani wa Yanga, Tarimba Abbas
ambaye pia kitaaluma ni mwanasheria ataongoza Kamati ya Nidhamu. Wajumbe
wanaounda kamati hiyo ni Wakili Jerome Msemwa (Makamu Mwenyekiti),
Kassim Dau, Nassoro Duduma na Kitwana Manara.
Kamati ya Rufani ya Nidhamu inaendelea
kuongozwa na Profesa Mgongo Fimbo wakati makamu wake ni Wakili Hamidu
Mbwezeleni. Wajumbe wengine wa kamati hiyo ni Titus Bandawe, Twaha
Mtengera na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) mstaafu Boniface Mpaze.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio
ambaye pia kitaaluma ni mwanasheria anaongoza Kamati ya Maadili. Wajumbe
ni Wakili Ezekiel Maganja, Wakili Victoria Mandari, Kanali mstaafu Enos
Mfuru na Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi, Said Mtanda.
Kamati ya Rufani ya Maadili inaundwa na
Jaji mstaafu Stephen Ihema (Mwenyekiti), Wakili Alesia Mbuya (Makamu
Mwenyekiti), Lilian Kitomari, Jabir Shekimweri na Chabanga Hassan
Dyamwale.
TFF, CRDB KUTATHIMINI TIKETI ZA ELEKTRONIKI
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeagiza kifanyike kikao cha dharura kati
ya Sekretarieti ya TFF, Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) na benki ya
CRDB ili kutathimini maendeleo ya matumizi ya tiketi za elektroniki.
Lengo la kikao hicho ni kutathimini
maendeleo ya utekelezaji wa mfumo huo wa tiketi za elektroniki ni
kutafuta ufumbuzi pamoja changamoto zake.
Viwanja vinane nchini vimefungwa mfumo
huo wa tiketi za elektroniki. Viwanja hivyo ni Uwanja wa Azam uliopo
Chamazi, Uwanja wa Kaitaba, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Uwanja wa
Jamhuri, Morogoro, Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Uwanja wa Sheikh
Kaluta Amri Abeid, Uwanja wa Mkwakwani, na CCM Kirumba.
MECHI YA STAND, KANEMBWA MEZANI TENA
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la
Mpira wa Tanzania (TFF) imeiagiza Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB)
ifanyie marejeo (review) uamuzi wake wa kuagiza mechi ya Ligi Daraja la
Kwanza (FDL) irudiwe mkoani Tabora.
Maagizo hayo yametolewa na Kamati ya
Utendaji iliyokutana jana (Februari 1 mwaka huu) baada ya kupokea
vielelezo vipya kuhusiana na mechi hiyo iliyochezwa Novemba 22 mwaka
jana mjini Shinyanga.
Mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Kambarage ilivunjwa na mwamuzi dakika ya 87 baada ya kupigwa na wachezaji wa Kanembwa JKT.
Pia Kamati ya Nidhamu ya TFF inatarajiwa
kukutana wiki ijayo kujadili tukio hilo la Shinyanga wakiwemo wachezaji
wanane wa Kanembwa JKT waliripotiwa kumpiga mwamuzi wa mechi hiyo.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
0 comments:
Post a Comment