Monday, 3 February 2014

MAMA SALMA:LINDI MSINDANGANYIKE NA WACHAFUNZI WA AMANI

 
WWWWWWWW_6d821.jpg
WAKAZI wa mkoa wa Lindi wametakiwa kutodanganyika na kundi la watu wachache, wanaotaka kuvuruga amani iliyopo, bali waitunze na kuhakikisha haipotei, kwani amani ikitoweka hao wanaowadanyanga, watakimbia na kuwaacha wakiteseka.
Wito huo ulitolewa  na Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) ya CCM wakati wa sherehe za Chama Cha Mapinnduzi (CCM) kutimiza miaka 37.

Sherehe hizo zilifanyika katika kata ya Kiwalala wilaya ya Lindi Vijijini.
Mama Kikwete alisema CCM imefanya mambo mengi katika harakati za ukombozi Barani Afrika, kwani Tanzania ilikuwa kimbilio la wanyonge kwa kuwa wapigania uhuru wengi kutoka nchi za Kusini mwa Afrika ambazo hazikuwa zimepata uhuru, walipokelewa , walihifadhiwa , walisaidiwa na kuwakarimu kwa dhati, jambo ambalo si dogo na hii yote ilitokana na amani iliyopo.
“Chama chetu kimefanya mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuleta demokrasia ya vyama vingi toka mwaka 1992 na leo hii tunatimiza miaka 22 ndani ya mfumo wa vyama vingi huku tukiwa na amani, umoja na ushikamano miongoni mwa watanzania, tumeleta usawa kwa wananchi wote bila kujali jinsia, rangi kabila wala dini. Chama cha Mapinduzi, kupitia Serikali zake, kinawajali wananchi kwa kuwasogezea huduma mbalimbali za kijamii hadi vijijini na kupanua fursa za kiuchumi na kimaendeleo kwa wananchi”, alisema Mke wa Rais.
Kwa upande wake, Mlezi wa Chama hicho Mkoa wa Lindi, Dk. Maua Daftari aliwataka wanachama wa chama hicho kuwa na umoja na mshikamano na kwa kufanya hivyo wataweza kushinda na kutekeleza ilani ya chama chao.
 CHANZO:HABARI LEO

Related Posts:

0 comments: