Monday, 3 February 2014

BIGI MECHI: MAN CITY v CHELSEA: ANGLIA VIKOSI, TAARIFA ILIYOTOLEA LEO NA TIMU ZOTE

negredo_c0345.jpg
>>MECHI: Jumatatu Februari 3 SAA 5 Usiku
>>UWANJA: Etihad
Usiku huu, Manchester City, ambao wako Nafasi ya Pili Pointi 2 nyuma ya Arsenal, na Chelsea walio Nafasi ya 3, Pointi 3 nyuma ya Man City, wanakutana kwenye Mechi ya Ligi Kuu England ambayo matokeo yake yatafafanua zaidi nini kitajiri mbio za Ubingwa Msimu huu.
Hii ni Mechi ya Pili kukutana Msimu huu na katika Mechi ya Kwanza huko Stamford Bridge, Chelsea waliibuka kidedea kwa Bao 2-1.
Lakini Man City, wakiwa kwao Etihad, ni mnyama mkali ambae anasaka ushindi wake wa 12 mfululizo na Msimu uliopita Uwanjani hapo Man City iliinyuka Chelsea Bao 2-0.
Kwenye Mechi hii, Timu zote zitawakosa Mastraika wao hatari, Sergio Agüero na Fernando Torres, ambao waliziona nyavu walipokutana Stamford Bridge mapema mwanzoni mwa Msimu huu.
Hali za Wachezaji:
Manchester City
-Majeruhi: García, Nasri, Agüero
-Mfungaji Bora: Agüero Bao 15
Chelsea
-Majeruhi: Torres, Van Ginkel
-Mfungaji Bora: Hazard Bao 9
Uso kwa Uso:
-Manchester City wameshinda Mechi 4 zilizopita dhidi ya Chelsea Uwanjani Etihad kuanzia Msimu wa 2008/09 na mara ya mwisho Carlos Tevez na Yaya Toure walifunga waliposhinda 2-0.
-Msimu huu, Chelsea iliifunga Manchester City Bao 2-1 Mwezi Oktoba kwenye Ligi kwa Bao za Andre Schurrle na Fernando Torres na Bao la City kufungwa na Sergio Aguero.
-Mara ya mwisho kwa Chelsea kuipiga City dabo, yaani Mechi zote mbili za Ligi katika Msimu mmoja, ni Msimu wa 2008/09.
VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
MAN_CITY_v_CHELSEA_TEAMS_3FEB
AKIBA:
Manchester City: Pantilimon, Nastasic, Clichy, Richards, Jovetic, Lescott, Rodwell, Boyata, Milner
Chelsea: Schwarzer, Hilário, Kalas, Cole, Ake, David Luiz, Mikel, Salah, Willian, Ba, Schürrle
Refa: Mike Dean

Related Posts:

0 comments: