Thursday, 20 February 2014

AMEIR PANDU KIFICHO,ATANGAZA TUME YA POSHO ZA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA

 

1(11)  Mwenyekiti wa Muda wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Pandu Ameir Kificho akiwashukuru wajumbe wa Bunge hilo baada ya kuchaguliwa.
………………………………………………………………               
NA MA GRETH KINABO- MAELEZO
Mwenyekiti wa muda wa Bunge Maalum la Katiba, Ameir Pandu Kificho, ametangaza tume ya sita kwa ajili ya kujadili kuhusu malalamiko ya posho ya Sh. 300,000 yaliyotolewa na baadhi ya   wajumbe wa Bunge Maalum ya Katiba kuwa haitoshi kuweza kuifanya kazi hiyo kwa umakini.
 Kificho  alitangaza majina hayo jana mjini Dodoma kabla ya kuanza kwa semina kwa wajumbe hao leo mjini Dodoma kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Bunge la Katiba Sura ya 83 toleo la mwaka 2014.
 “Kuhusu suala la kumudu kuishi vizuri na hii kazi nzito tuliyonayo bado halina majibu kwa sasa ,” alisema Mwenyekiti huyo.
 Aliyataja majina hayo kuwa ni William Lukuvi, Mohammed Aboud   Mohammed,   Freeman Mbowe ,Paul  Kimiti , Asha Bakari Makame na  Jenista  Mhagama.
 Alisema timu hiyo itakutana mara baada ya semina hiyo  leo na ikiongozwa na Mwenyekiti huyo wa muda ili kuweza kukaa pamoja na kupanga  ya kuweza kuiomba  Serikali  kuangalia jambo hilo na kuweza kupata majibu.
 Timu hiyo imeundwa baada ya baadhi ya wajumbe  wa bunge hilo kulalamikia posho hizo ndani na nje ya ukumbi wa Bunge jana.

Related Posts:

0 comments: