Thursday, 20 February 2014

KAIMU MWAKILISHI MKAZI WA UNFPA ATEMBELEA OFISI YA RAIS, TUME YA MIPANGO

Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Masuala ya Idadi ya Watu (UNFPA), Bibi Mariam Khan leo alitembelea Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango na kutoa wito kwa serikali kufanya hima katika kukabiliana na changamoto za ongezeko la idadi ya watu na ukuaji wa mijini nchini Tanzania.

Hata hivyo, Bibi Khan alisema kuwa licha ya kuwa ongezeko la idadi ya watu linaathari mbalimbali kama lisipothibiwa, Tanzania inaweza kutuma fursa hiyo kwa kuwekeza kwa vijana kama nguvu kazi kwa shughuli za kimaendeleo ili kuongeza pato na uchumi wa taifa.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Dkt. Philip Mpango alisema kuwa serikali inatambua changamoto hizo, na kuwa kwa sasa inajipanga kuipitia Sera ya Idadi ya Watu ya Mwaka 2006 ili iendane na changamoto hizo.
????????

Related Posts:

0 comments: