SOMA ZAIDI:
GIROUD FITI KUIVAA VILLA LEO
Giroud alikuwa nje tangu afunge Bao la
Ushindi Arsenal ilipoichapa Newcastle United Bao 1-0 hapo Desemba 29
baada kupata Jeraha na kuchanika Enka yake.
Nicklas Bendtner aliumia hapo Januari 1
wakati akifunga kwenye Mechi na Cardiff City waliposhinda 2-0 na
anatarajiwa kuwa nje kwa Wiki kadhaa wakati Theo Walcott aliumia vibaya
Goti kwenye Mechi iliyofuatia ya FA CUP waliyoifunga Tottenham 2-0 na
atakuwa nje kwa Miezi 6.
Lakini hivi karibuni, Straika wa Germay Lukas Podolski alirejea Uwanjani baada kuwa nje kwa Miezi kadhaa akijiuguza Mguu wake.
AC MILAN: MASSIMILIANO ALLEGRI AFUKUZWA!
Siku moja baada kuchapwa 4-3 na ‘Timu mbovu’ Sassuolo, Vigogo wa Italy, AC Milan, wameamua kumtimua Kocha wao Massimiliano Allegri.
AC Milan, ambao wameshawahi kuwa
Mabingwa wa Italy mara 18, wapo Nafasi ya 11 kwenye Ligi ya Serie A na
wapo Pointi 30 nyuma ya Vinara Juventus.
Allegri, mwenye Miaka 46, ambae
alitarajiwa kuondoka mwishoni mwa Msimu baada Mkataba wake kumalizika,
ametimuliwa pamoja na Wasaidizi wake wote.
Kocha Msaidizi Klabuni hapo, Mauro
Tassotti, ambae ni Mchezaji wa zamani wa AC Milan, amepewa kazi ya
kukaimu Nafasi iliyoachwa wazi.
Tassotti, mwennye Miaka 53, alikaa kwa Miaka 17 kama Mchezaji hapo Sa Siro na amekuwa Kocha hapo tangu astaafu Soka Mwaka 1997.
Klabu nyingine ya Serie A ambayo
imemtimua Meneja wake hii leo ni Livorno ambao wako Nafasi ya 19 na
wamemfukuza kazi Davide Nicola.
SAMIR NASRI: NJE WIKI 8!
Kiungo wa Manchester City Samir Nasri
leo amethibitishwa kuwa atakuwa nje ya Uwanja kwa Wiki 8 baada kuumia
Goti hapo Jana huko Saint James Park walipoifunga Newcastle Bao 2-0
kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.
Nasri aliumizwa alipopigwa Buti Gotini na Mapou Yanga-Mbiwa ambae alipewa Kadi ya Njano kwa kitendo hicho.
Akithibitisha habari hizi kwenye Mtandao
wake wa Twitter, Nasri aliposti: “Nadhani ni habari njema kuwa nje Wiki
8. Asante wote kwa kunipa sapoti na kunitakia mema!”
Mara baada ya Mechi ya Jana, Meneja wa
City, Manuel Pellegrini, alionyesha wasiwasi wake aliposema Nasri
ameumia vibaya lakini hii leo, baada uchunguzi wa kina, imethibitika
maumivu yake si mabaya sana.
0 comments:
Post a Comment