Saturday, 8 February 2014

ANDY CARROLL-KIFUNGO: WEST HAM YAGONGA MWAMBA!

ANDY CARROLL-KIFUNGO: WEST HAM YAGONGA MWAMBA!
>>RASMI KUZIKOSA MECHI 3!
ANDY_CARROLL_v_CHICO_FLORESKIFUNGO cha Mechi 3 kwa Andy Carroll kimebaki pale pale baada ya Jopo Huru kuafiki kuitupa Rufani ya West Ham kupinga Adhabu hiyo.
West Ham, baada ya Rufaa yao kukataliwa na FA, ilitishishia kwenda Mahakamani na FA ikabidi iitishe Jopo maalum.
SOMA HABARI ZA AWALI:
ANDY CARROLL-KIFUNGO: FA YASALIMU AMRI KWA WEST HAM!
>>YAITISHA KIKAO CHA USULUHISHI KUKWEPA MAHAKAMA!
BAADA West Ham kutaka kuchukua hatua za Kisheria, kitu ambacho hakijapata kufanyika huko England, FA imesalimu amri na kuitisha Kikao cha Usuluhishi hii Leo Asubuhi ili kujadili Adhabu ya Kufungiwa Mechi 3 kwa Straika Andy Carroll baada kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu Wikiendi iliyopita kwenye Mechi na Swansea City.
West Ham United ilitishia kuchukua hatua za Kisheria dhidi ya FA ikiwa watakataa kumkubalia Straika wao Andy Carroll kupewa nafasi nyingine ya kujitetea baada ya Rufaa yake kupinga Kadi Nyekundu kutupwa nje na Jopo Huru la FA na hivyo kufungiwa Mechi 3.
Kwa mujibu wa Kanuni za FA, Chama cha Soka England, uamuzi wa Jopo Huru ni wa mwisho na hauwezi kukatiwa Rufaa nyingine.
Ili kuepusha suala hili kwenda Mahakamani, FA itakuwa na Kikao hii Leo kitakachoendeshwa na Jopo la Watu Watatu ambapo FA na West Ham zitachagua Memba mmoja na Mwenyekiti atakubaliwa kati yao.
Carroll alipewa Kadi hiyo Jumamosi wakati Timu yake inaichapa Swansea City Bao 2-0  na kuonekana na Refa Howard Webb kuwa alimpiga kipepsi Beki wa Swansea Chico Flores ingawa marudio ya tukio hilo yalionyesha Beki huyo hakupigwa bali aliparazwa na mkono wa Carroll juu ya kichwa waliporuka wote juu.
Kifungo hicho kitamfanya Andy Carroll azikose Mechi 3 muhimu za West Ham ambao wanapigania kukwepa kuburutwa kwenye vita ya kushuka Daraja.
Mechi ambazo atazikosa Carroll ni zile na Aston Villa, huko Villa Park Siku ya Jumamosi, na zile za Nyumbani Uwanjani Upton Park dhidi ya Norwich na Southampton.
Akiongelea ishu hii ya Carroll, mmoja wa Wamiliki wa West Ham, David Gold, alisema wao wamelazimika kutaka kuchukua hatua za Kisheria kwa vile hamna njia nyingine ya kufanya.
Alisema: “Hamna pa kwenda. Kilichobaki kuchukua hatua za Kisheria. Si kitu bora sana kwani hili ni suala la Soka. Kama tungekuwa katikati kwenye Msimamo wa Ligi pengine tungelipuuza lakini tunapigania uhai wetu kubaki Ligi Kuu. Hapa kila Mtangazaji wa Soka na Asilimia 80 ya Wanahabari wanasema ile sio Kadi Nyekundu!”

Related Posts:

0 comments: