
Mmoja kati ya majeruhi wa ajali za boda boda Iringa aliyepata ajali wakati wa mapokezi ya waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa mwaka jana |
Madereva boda boda waliopewa mafunzo na kamati ya usalama barabarani mjini Iringa wakila kiapo |
Majeruhi wa bado boda aliyevunjika mguu kwa ajili ya bodaboda wakati wa mkesha wa Mwaka mpya 2014 akiwa Hospital ya rufaa ya mkoa wa Iringa |
![]() |
Hii ni ajali ya pikipiki iliyotokea wakati wa mapokezi ya Lowassa Iringa mwaka jana |
Rais Dr Jakaya Kikwete akisalimiana na mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa Iringa Salim Asas kulia |
Naibu meya wa manispaa ya Iringa Bw Gervas Ndaki akitazama ajali mbaya ya gari eneo la CRDB ya Zamani mjini Iringa |
![]() |
Mfanyabiashara wa zamani Bw Makosa akiwa juu ya magari yaliyopata ajali |
RPC Mungi akiwa na mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani Bw Asas kulia siku walipofunga mafunzo kwa madereva bodaboda mjini Iringa
.......................................................................................................................
TAKWIMU za jeshi la polisi mkoani Iringa zinaonyesha kwa mwaka 2013 idadi ya vifo vya ajali za barabarani imeshuka ukilinganisha na mwaka 2012 ambapo watu 157 walipoteza maisha kwa ajali za barabarani huku mwaka 2013 ni watu 123 ndio waliopoteza maisha kwa ajali za barabarani.
Mbali
ya takwimu kuonyesha kupungua kwa vifo vya ajali za barabarani
zinazotokana na magari bado kumekuwepo kwa ongezeko la ajali 21 za
pikipiki kati ya mwaka 2012 ambao ulikuwa na ajali 21 huku mwaka
2013 ajali zikifikia 42 wakati vifo vya ajali za pikipiki
zikiongezeka kutoka 10 mwaka 2012 hadi vifo 23 mwaka 2013.
Akitoa
taarifa ya tathimini ya ajali kwa mwaka 2012 na 2013 wakati
akizungumza katika mahojiano maalum mtandao wa www.matukiodaima.com leo ,kamanda wa
polisi wa mkoa wa Iringa ,Ramadhan Mungi alisema kuwa ajali za
pikipiki zimeonyesha kuongezeka pamoja na jitihada kubwa
zinazofanywa na kamati ya usalama barabarani mkoa wa Iringa chini
ya mwenyekiti wake Salim Asas ambae amekuwa akitoa mafunzo ya mara
kwa mara kwa madereva boda boda.
Kamanda
Mungi alisema kuwa kwa mwaka 2012 jumla ya makosa ya usalama
barabarani 21267 yalipatikana na mwaka 2013 makosa ya usalama
barabarani yalikuwa 28705 wakati faini zitokanazo na makosa hayo
zilipatikana kiasi cha zaidi ya Tsh milioni 6. 4 kwa mwaka 2012 na
mwaka 2013 faini ilikusanywa kiasi cha zaidi ya Tsh milioni 8.9 ikiwa
ni ongezeko la zaidi ya Tsh milioni 2.4 ukilinganisha na mwaka 2012.
Alisema
kuwa kwa upande wa ajali zilizotokana na magari mbali ya watu 123
kupoteza maisha kwa mwaka 2013 bado kulikuwa na upungufu wa majeruhi
20 ukilinganisha na mwaka 2012 ambapo majeruhi walikuwa 140 na mwaka
2013 majeruhi walikuwa 120
Wakati
kwa ajali zitokanazo na pikipiki mwaka 2012
majeruhi walikuwa ni 14 ila mwaka 2013 majeruhi wa ajali za
pikipiki walikuwa 23 hivyo inaonyesha ni kiasi gari mwaka 2013
ambapo ajali za pikipiki zilivyochangia idadi kubwa ya majeruhi .
Hata
hivyo alisema inashangaza kuoana jitihada kubwa zinafanywa na
kamati ya usalama barabarani katika kutoa mafunzo kwa madereva boda
boda ila bado ajali kwao zinazidi kuongezeka zaidi.
Kwani
alisema kwa mwaka 2012 ni madereva 400 ndio walipewa mafunzo huku
mwaka 3012 jumla ya madereva pikipiki 900 walipatiwa
mafunzo ya usalama barabarani ila bado ajali zimeongezeka badala
ya kupungua.
0 comments:
Post a Comment