Mweka Hazina
wa Chama Cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini (Taswa), Sultan
Sikilo amefariki dunia na atazikwa leo katika makaburi ya Kibada,
Kigamboni katika Manispaa ya Temeke.
Ikumbukwe
kuwa marehemu alichaguliwa miaka mitatu iliyopita na enzi za uhai wake
alipitia nafasi mbali mbali katika chama ikiwa pamoja na ujumbe.
Marehemu pia alikuwa Mweka Hazina wa Timu ya waandishi wa habari za
michezo nchini (Taswa SC).
Kutokana na
msiba huu, tunawaomba waandishi wa habari za michezo nchini, wadau na
jamii kwa ujumla kuwa karibu na familia yake katika kipindi hiki kigumu.
Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Sultani Sikilo Peponi, Amina.
Majuto Omary
Mwenyekiti Taswa SC
0 comments:
Post a Comment