’ PAMOJA NA WAPINZANI!’
Hiyo Jana Moyes alitamka: “Sasa inabidi tucheze dhidi ya Marefa na Timu pinzani. Ni mbaya sana. Tumeanza kuwacheka.”
Moyes alikuwa amekerwa na uamuzi wa Refa
Andre Marriner kuipa Sunderland Penati iliyozaa Bao lao la Pili na vile
vile kuwapa Frikiki iliyoleta Bao lao la kwanza.
Refa Andre Marriner hakuashiria Penati
hiyo lakini ilibidi aitoe baada ya ushauri kutoka kwa Mshika Kibendera
wake baada Adam Johnson kuanguka wakati akikabiliana na Tom Cleverley.
Kuhusu Sunderland kupewa Penati Jana,
Moyes alihoji: “Itakuwaje Mshika Kibendera atoe Penati? Refa alikuwa
akiangalia moja kwa moja tukio lile lakini Mshika Kibendera alikuwa
haoni kwani kazibwa na Evra! Mchezaji wetu sisi alipewa Kadi kwa tukio
kama hilo walilopewa Penati! Hata lile Bao la kwanza ile haikuwa Frikiki
ingawa ni kosa letu kutojilinda vizuri kwa Frikiki ile na kuruhusu
Bao!”
Wiki iliyopita, Moyes pia alilalamika
kuhusu Marefa wakati Man United ilipofungwa na Tottenham Bao 2-1 kwenye
Ligi na Refa Howard Webb kuwanyima Penati ya wazi kabisa.
0 comments:
Post a Comment