Wednesday, 8 January 2014

MCHEZAJI AKIRI YEYE NI SHOGA,NA DOKTA ADAI UWEZO KUMPONYA WALCOTT ACHEZE BRAZIL!!

 RODGERS ASALIMU AMRI KWA FA, ANGOJA ADHABU TU!
WALCOTT_NA_ISHARAWAKATI Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Germany akikiri kuwa ni Shoga, yupo Daktari kutoka Scotland amedai anaweza kumponya Theo Walcott ndani ya Miezi minne ili awahi kucheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwezi Juni na Meneja wa Liverpool, Brendan Rodgers, amekiri Kosa kwenye Mashitaka yake toka FA.

MCHEZAJI AKIRI SHOGAThomas_Hitzlsperger
Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Germany, Thomas Hitzlsperger, amekiri kuwa yeye ni Shoga.
Hitzlsperger, mwenye Miaka 31 na ambae amestaafu Soka Mwezi Septemba, aliichezea Germany mara 52 kati ya Miaka ya 2004 na 2010 na pia kuzichezea Klabu za Aston Villa, VfB Stuttgart, Lazio, West Ham United, VfL Wolfsburg na Everton.
Huku akiungwa mkono na Viongozi wa Serikali za Germany, Hitzlsperger amedai ameamua sasa kujitokeza ili kutetea Mashoga kwa Wanamichezo.
DOKTA AWEZA KUMPONYA WALCOTT NDANI YA MIEZI MINNE ILI ACHEZE BRAZIL!
Daktari Bingwa kutoka Scotland yupo mbioni kuwasiliana na Arsenal ili kumuokoa Mchezaji wao Theo Walcott kukosa kuchezea England kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwezi Juni.
Walcott, ambae aliumia Goti Jumamosi iliyopita Arsenal walipoifunga Tottenham Bao 2-0 kwenye FA CUP, ametangazwa kuwa atakuwa nje ya Uwanja kwa Miezi 6.
Lakini Profesa Gordon Mackay amedai kuwa atatumia mbinu mpya ya kumponya Walcott ndani ya Miezi minne na hivyo kuweza kuwahi kucheza huko Brazil.
Profesa huyo, ambae hutumia utaalam wa kuingiza sapoti kwenye Goti na hivyo kuruhusu Mazoezi ya mapema huku Goti likipona wenyewe, amedai ndani ya Wiki 12 Walcott ataweza kuanza kufanya Mazoezi ya kukimbia.
Profesa Mackay ameshawahi kuwatibu Wanamichezo kadhaa, akiwemo Mcheza Raga wa Scotland Max Evans, ambae alirudi Uwanjani mapema mno kupita matibabu ya kawaida yanavyoruhusu.
RODGERS AKIRI KOSA KWA FA
Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers amekiri kosa lake kufuatia Mashitaka yake ya kumponda vibaya Refa Lee Mason na kusema maamuzi yake yalikuwa ya ‘kutisha’ mara baada ya kufungwa Bao 2-0 na Man City Uwanjani Etihad Wiki iliyopita.
Sasa Rodgers itabidi asubiri adhabu yake ambayo inatarajiwa kuwa Faini.
Akiongea baada ya Mechi hiyo, Brendan Rodgers, alisema: “Nasikia fahari kwa Wachezaji wangu. Walicheza vizuri mno. Lakini hawakupata msaada wowote toka kwa Waamuzi. Nadhani walifanya maamuzi ya kutisha. Hatukupata lolote toka kwao. Yule Mshika Kibendera wa upande mmoja alishindwa kuwa mstari sawa na Wachezaji. Ukifanya kazi hii ya kiwango cha juu ni lazima uwe na maamuzi sahihi. Ile alipewa Ofsaidi [akimaanisha Bao la Raheem Sterling lililokataliwa] wakati si sahihi. Ni maamuzi makubwa kwenye Mechi!”
Vile vile, Brendan Rodgers alihoji eneo alilotoka Refa Lee Mason, ambae ni Mkazi wa Bolton, eneo ambalo liko Maili 16 tu toka Uwanja wa Etihad na kutaka asipewe Mechi za Klabu za Jiji la Manchester.
Alisema: “Kulikuwa na Penati ya Suarez. Natumai hatupati tena Refa wa Eneo la Manchester katika Mechi nyingine ya Liverpool-Manchester City!”
Baadae, Rodgers alijaribu kujitetea pale aliposema: “Hakika sikuwa nahoji uadilifu wa Marefa. Ilikuwa ni kitu sahihi kuuliza Refa wa eneo hilo hilo kupewa Mechi Manchester!”
Rodgers alipewa hadi leo Januari 8 Saa 3 Usiku kujibu Mashitaka hayo.

0 comments: