Thursday, 9 January 2014

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA AKIONYA CHAMA CHA CHADEMA


                                                    
 jaji  Francis Mutungi

                      Na Amina Azizi wa radio uhuru Fm, Dar es Salaam 
                   Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Jaji FRANCIS MUTUNGI, amekemea vurugu na vitendo vya uvunjifu wa amani vilivyotokea maeneo ya Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es salaam, baada ya kusikilizwa na kutolewa uamuzi wa kesi ya ZITO KABWE.

          Kauli hiyo imekuja kufuatia hivi karibuni wafuasi wanaomuunga mkono ZITTO na wengine uongozi wa CHADEMA kufanya vurugu katika maeneo ya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.

         Jaji MUTUNGI amekemea suala hilo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa leo, kuhusu vitendo vya vurugu vilivyotokea katika maeneo ya Mahakama hiyo baada ya kusikiliwa na kutolewa uamuzi wa kesi ya ZITTO dhidi ya CHADEMA.

         Kupitia taarifa hiyo Jaji MUTUNGI amewaasa viongozi wa CHADEMA na ZITTO kuzuia wafuasi wao kujihusisha na vitendo vya vurugu na uvunjifu wa amani wa aina yoyote wakati wote ambapo mgogoro baina yao ukiwa bado unaendelea.

          Amesema migogoro ndani ya vyama vya siasa ni moja wapo ya vyanzo vya uvunjifu wa amani hivyo amewaasa wadau wote kwamba migogoro hiyo inapaswa isivuke mipaka na kuwa uhasama na uadui wa kufanya wafuasi wa pande mbili kupigana kwani hiyo sio demokrasia.

          Hata hivyo amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuonyesha ukomavu wa kisiasa kwa kushughulikia tofauti zao na migogoro baina yao kwa ustaarabu, utulivu na amani huku wakizingatia sheria zote za nchi.

          Sheria ya Vyama vya Sisa namba 5 ya mwaka 1992 na kanuni za maadili ya vyama vya siasa za mwaka 2007 inakataza vyama vya siasa kuruhusu wanachama au mashabiki wake kujihusisha na vitendo vya vurugu na uvunjifu wa amani wa aina yoyote ile.

 

Related Posts:

0 comments: