>>KWENYE MALENGO YA MAN UNITED YUPO PIA TONI KROOS!
Cardiff City, ikiongozwa na Nguli wa
zamani wa Man United, Ole Gunnar Solskjaer, ipo katika hatua za mwisho
kuwanasa Vijana wa Man United, Fabio na Zaha, ili wacheze kwa Mkopo hadi
mwishoni mwa Msimu.
Zaha, ambae alinunuliwa kutoka Crystal
Palace, ameichezea Man United Mechi 4 tu Msimu huu na kwenda kwake
Cardiff kutampa nafasi ya kuchezea Timu ya kwanza.
Nae Fabio, ambae Msimu uliopita alikuwa
QPR kwa Mkopo, anahitaji pia kucheza mara kwa mara tofauti na Pacha
mwenzake, Rafael, ambae hucheza Timu ya Kwanza ya Man United.
Mapacha hao, wenye Miaka 23, walijiunga na Man United Mwaka 2008 wakitokea Klabu ya kwao Brazil, Fluminese.
Cardiff, ambao Jumanne watatua Old
Trafford kucheza na Man United kwenye Mechi ya Ligi, pia wapo hatua za
mwisho kumsaini Kenwyne Jones kutoka Stoke City kwa kubadilishana na
Peter Odemwingie ambae atakwenda Stoke.
WAKATI HUO HUO, zipo
ripoti kuwa Man United wanatafakari kumnunua Kiungo toka Ufaransa
anaechezea Newcastle, Yohan Cabaye, ambae anathaminiwa kuwa na Dau la
Pauni Milioni 25.
Lakini Cabaye pia yumo kwenye macho ya Arsenal na Paris Saint-Germain ingawa Klabu hizo zinadaiwa kumtaka kwa Dau hafifu.
PSG inasadikiwa iko tayari kumnunua kwa
Pauni Milioni 17 wakati Arsenal wameshawahi kukataliwa Ofa yao ya Pauni
Milioni 10.2 waliyotoa mwanzoni mwa Msimu.
Mbali ya Cabaye, Meneja wa Man United,
David Moyes, pia anadaiwa kuwa na nia ya kumchukua Kiungo wa Bayern
Munich, Toni Kroos, ambae alikwenda kumtazama akicheza wakati Bayern
Munich inaifunga Borussia Monchengladbach Bao 2-0 Juzi Ijumaa huku Moyes
akinaswa akiongea na Wakala wa Kroos, Sascha Breese.
Hivi sasa Kroos, ambae Mkataba wake na
Bayern unamalizika mwishoni mwa Msimu ujao, yupo kwenye mvutano na Klabu
yake kuhusu Mkataba mpya na inaaminika anaweza kuihama hivi sasa kwa
Dau la kati ya Pauni Milioni 20 hadi 25.
0 comments:
Post a Comment