Thursday, 23 January 2014

CHELSEA ‘YAIPINDUA’ LIVERPOOL KUMNASA MMISRI! MOHAMED SALAH

>>YAFANYA WALICHOWAFANYIA SPURS KWA WILLIAN!
>>CHELSEA YAKUBALIANA NA BASEL KUMSAINI MOHAMED SALAH WA MISRI!
>>SASA DILI YA MATA KUTANGAZWA RASMI!
Mohamed_SalahChelsea imekubaliana na FC Basel kumsaini Winga wa Egypt Mohamed Salah kwa Dau linaokadiriwa kuwa ni Pauni Milioni 11.
Salah, Miaka 21, bado hajapimwa Afya wala kukubaliana Maslahi yake binafsi na Chelsea lakini anatarajiwa kuhamia Stamford Bridge.
Ilikuwa sio siri kuwa Liverpool ndio walioanza mazungumzo na Basel, Mabingwa wa Uswisi, ili kumchukua Salah lakini sasa Chelsea wamefanya kile kilichowakuta Tottenham ‘waliponyang’anywa’ Kiungo Willian kutoka Anzhi ya Urusi Dakika za mwisho.
Jana Chelsea ilifikia Makubaliano na Manchester United kuwauzia Juan Mata na Dili hii ilicheleweshwa kuthibitishwa na Klabu hizo mbili ikiaminika Chelsea wanangoja kukamilisha Uhamisho wa Salah ili Uhamisho wa Mata utangazwe rasmi!
Salah anakuwa Mchezaji wa Pili Chelsea kumsaini kwenye Dirisha la Uhamisho la Januari na mwingine ni Nemanja Matic aliesaini kwa Pauni Milioni 21 kutoka Benfica Wiki iliyopita.
Salah, ambae aliifunga Bao Chelsea walipocheza na Basel kwenye Nusu Fainali ya Europa Ligi Msimu uliopita na pia kuiipiga Bao kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu huu, anang’ara mno huko Uswisi na amekuwa akiwindwa na Klabu kubwa Barani Ulaya.


EXCLUSIVE: CHELSEA YAIPIGA CHINI LIVERPOOL NA KUFANIKIWA KUMSAJILI MSHAMBULIAJI WA FC BASLE MOHAMMED SALAH.


Klabu ya Chelsea imefanikiwa kuipiku Liverpool na kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Fc Basle ya nchini Uswizi raia wa Misri,Mohammed Salah kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 1.
Salah maarufu kama Messi wa Misri kwa muda mrefu alikuwa akiwaniwa na Liverpool.

0 comments: