Mahmoud Ahmad
Wakazi
wa kata ya mbugani mtaa wa mabatini kaskazini eneo la mwembe giza
wamekiomba chama cha mapinduzi katika kata hiyo na wafadhili
mbalimbali hapa nchini kuwasaidia mchango wa hali na mali katika
kufanikisha upatikanaji wa huduma ya umeme kwenye eneo lao kwa
kuwasaidia mchango wa kupata nguzo tano kati ya saba zinazohitajika.
Wakiongea
kwenye kikao chao cha ukusanyaji wa michango ya kupata huduma hiyo ya
umeme mbele ya katibu wa ccm wa kata hiyo Gerald Mashala wakazi hao
wamemuelezea kuwa wamejitahidi kukusanya fedha za kununulia nguzo mbili
hadi sasa lakini kutokana kipato chao kuwa kidogo wanakiomba chama cha
mapinduzi kuwasaidia upatikanaji wa nguzo tano iliwaweze kusogeza huduma
hiyo.
Pia
wakawataka wafadhili mbalimbali kusaidia upatikanaji wa hizo nguzo
tano za umeme ilikuweza kupata urahisi wa ufikaji wa eneo hilo kwani kwa
kipindi hichi wazee,wagonjwa na walemavu wamekuwa wakipata tabu
kutokana na giza na ufikaji wa eneo lao kwani lipo milimani.
“Unajua
ndugu mwandishi eneo letu lipo milimani na tunaishi na wazee,walemavu
na saa zingine wagonjwa na wajawazito kwa hali hii ni hatari kubwa sana
nyakati za usiku ufikaji wakeunakuwa wa shida hivyo kupitia wewe
tunaomba kupatwa huduma hiyo kwa haraka”alisisitiza Peter.
Hata hivyo CCM
kata hiyo imeahidi kutoa kiasi cha sh.200,000 katika jitihada za
kufanikisha juhudi za kujiletea maendeleo kwani wameonyesha juhudi kubwa
na hiyo ni kusaidia ilani ya chama hicho kufikisha asilimia
30%wawewamefikishiwa huduma ya umeme kwwa nchi nzima.
Mashalla
pia akasema atasaidia kwenda wafadhili mbalimbali wenye moyo wa
kusaidia maendeleo ilikuwezesha upatikanaji wa huduma hiyo huku
akiyaomba makampuni mbalimbali kusaidia kwa karibu jamii za pembezoni
ilikuweza kujiona hawajatengwa na jamii.
“Unajua
wakazi hawa ni sehemu ya wakazi wa kata hii wanaohitaji huduma
mbalimbali za kijamii ikiwemo huduma hii ya umeme na maji kwani
limekkuwa ni tatizo sugu huku mamlaka husika zikishindwa kukaa na jamii
kujua zitasaidiaje na hili ni tatizo”alisema mashalla.
0 comments:
Post a Comment