Saturday, 15 February 2014

VIKWAZO DHIDI YA IRANI VYA SABABISHA MATATIZO AFRIKA KUSINI

    Maite-Nkoana-Mashabane-e1351665718872_d3f7c.jpg

Athari mbaya itokanayo na vikwavo vya upande mmoja vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimelalamikiwa vikali na viongozi wa Afrika Kusini. Naibu Katibu Mkuu wa Idara ya Mambo ya Asia na Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo, sambamba na kusema kuwa Iran imepiga hatua kubwa katika teknlojia za kisasa na viwanda vya madawa amesema kuwa, maendeleo ya Iran katika nyuga za elimu na teknolijia, hususan katika masuala ya nyuklia, yanakwenda kwa kasi sana. Amesema kuwa, walimwengu wamekubali kwamba, kufanya mazungumzo na Iran ni kwa manufaa ya pande zinazofanya mazungumzo hayo. Itakumbukwa kuwa, Waziri wa Mambo ya Nje ya Afrika Kusini, Bi Maite Nkoana-Mashabane hivi karibuni alisema
kuwa nchi yake iko tayari kuanza kununua mafuta ghafi kutoka Iran na kuongeza kuwa, vikwazo vilivyowekwa dhidi ya Tehran, vimekuwa na taathira mbaya kwa uchumi kwa nchi mbalimbali za dunia. Mashabane amesisitiza kuwa, kuna udharura wa kuondolewa vikwazo hivyo visivyo na msingi kwa ajili ya maslahi ya walimwengu. Amesisitiza kuwa, viwanda kadhaa nchini Afrika Kusini vimepata hasara kubwa katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na kuzuiliwa kununua mafuta ya Iran.
Chanzo, kiswahili.irib.ir/habari

Related Posts:

0 comments: