RASMI ZAPANGWA KWENYE VYUNGU VYA DROO!
Fainali hizo zenye Nchi 32 zitapangwa katika Makundi 8 ya Timu 4 kila moja.
Katika mwongozo huo, FIFA imesema Timu 8
 za juu kwa Ubora Duniani [Kwa mujibu wa Listi iliyotoka Oktoba], pamoja
 na Wenyeji Brazil, zipo Chungu Namba 1 na zitapangwa kuanzia Kundi A 
hadi H ili kuzitenganisha.
Brazil, kama Wenyeji, tayari wamewekwa 
Kundi A na watacheza Mechi ya Ufunguzi ya Fainali za Kombe la Dunia hapo
 Juni 12 huko Sao Paulo.
-CHUNGU NAMBA 1: Brazil, Spain, Argentina, Belgium, Colombia, Germany, Switzerland, Uruguay
-CHUNGU NAMBA 2: Ivory Coast, Ghana, Algeria, Nigeria, Cameroon, Chile, Ecuador
-CHUNGU NAMBA 3: Japan, Iran, South Korea, Australia, United States, Mexico, Costa Rica, Honduras
-CHUNGU NAMBA 4: Bosnia, Croatia, England, Greece, Italy, Netherlands, Portugal, Russia, France
FAHAMU: Kabla Droo 
kufanyika itafanyika Droo maalum kuihamisha moja ya Timu za Ulaya toka 
Chungu Namba 4 na kuiweka Namba 2 ili kuleta uwiano wa Nchi toka Mabara 
tofauti.
Pia, Timu 4 za kutoka Marekani ya 
Kusini, Brazil, Uruguay, Colombia na Argentina zitawekwa kwa muda Chungu
 Namba X. Timu 3 ambazo hazitapangiwa ile Timu ya Ulaya ambayo 
ilipelekwa Chungu Namba 2 zitarudishwa kwenye Droo kubwa kama 
walivyopangiwa awali.
 






 
 
 
 






0 comments:
Post a Comment