Monday, 10 February 2014

VIKAO VYA MAHAKAMA KUU KANDA YA KATI KUANZA LEO

 
majaji 1
Jaji Othman Chande 
Na Nathaniel Limu, Singida
VIKAO vya mahakama kuu kanda ya kati vinatarajiwa kuanza leo februari 10 hadi machi 11 mwaka huu mjini hapa.
Akizungumza na MOblog hivi karibuni, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mwandamizi,Joyce Minde amesema vikao hivyo vitakavyofanyika kwenye mahakama ya wazi ya hakimu mkazi mjini Singida.
Minde amesema vikao hivyo vitakuwa chini ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu kanda ya kati,Cresentia Makuru.
Amesema jumla ya kesi 18 za mauaji zitasikilizwa,wakati kesi zingine 19,zitasomwa katika hatua ya awali.
Minde amesema kuwa kabla ya kuanza kwa vikao hivyo,jaji Makuru atakagua gwaride rasmi la kuashiria kuanza kwa vikao vya mahakama kuu kanda ya kati mkoani Singida,kwa kipindi cha mwaka huu.

Related Posts:

0 comments: