TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE JIMBO LA KALENGA
Tume ya Tifa ya Uchaguzi imepokea barua kutoka kwa Mhe. Spika wa BUNGE la Jamhuri ya Muungano Tanzania ya kuiarifu uwepo wa nafasi wazi ya Ubunge katika Jimbo la Kalenga lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Vijijini, kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. William Mgimwa aliyefariki dunia tarehe 1/1/2014. Baada ya taarifa hiyo Tume imepanga ratiba ya Uchaguzi mdogo katika Jimbo la Kalenga kama ifuatafyo:-
- Uteuzi wa Wagombea Ubugne utafanyika tarehe 18-Februari-2014
- Kampeni za Uchaguzi zitaanza tarehe 19-Februari-2014 hadi 15-Machi-2014
- Siku ya kupiga kura ni Jumapili terehe 15-Machi-2014
Tume inawasisitiza wananchi wote katika maeneo husika kujitokeza kukagua tarifa zao wakati wa kuweka wazi Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili kuona kama kuna marekebisho madogo yanahitajika kufanyika kuwawezesha kupiga Kura bila malalamiko yoyote. Ikumbukwe kwamba hakutakuwa na uandikishaji mpya wa Wapiga Kura.
J. Mallaba
MKURUGENZI WA UCHAGUZI
0 comments:
Post a Comment