Kada wa Chadema na muuza magazeti maarufu mkoa wa Iringa Aidan Pugili kushoto akirejesha fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania ubunge jimbo la Kalenga leo jioni kwa viongozi wa Chadema wilaya ya Iringa vijijini kesho wana Chadema jimbo la Kalenga watashiriki kupiga kura za maoni kuteua mgombea katia ya wanachama 13 waliojitokeza
Katibu wa Chadema wilaya ya Iringa vijijini Felix Nyondo akitangaza majina ya waliojitokeza kuchukua fomu leo
Baadhi ya wanachama wa Chadema wakiwa ofisi za chama hicho eneo la Kichangani mjini Iringa
CHAMA
Cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) wilaya ya Iringa vijijini
kimepongeza mwitikio mzuri wa wanachama wake 13 akiwemo kijana kada na
muuza magazeti maarufu mkoani Iringa Aidan Pungili kwa kujitokeza
kuchukua na kurejesha fomu za kuomba kuteuliwa kugombea kumrithi
aliyekuwa mbunge wa jimbo la Kalenga marehemu Dr Wiliam Mgimwa
Katibu
wa Chadema wilaya ya Iringa vijijini Felix Nyondo alisema kuwa
zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu kwa wanachama wake
lilimalizika jana majira ya saa 10 jioni kwa wanachama wake wote
waliojitokeza kuchukua fomu kurejesha fomu hizo kwa wakati.
Hata
hivyo alisema kuwa kumekuwepo na mwitikio mkubwa wa makada maarufu
waliokuwepo katika vyama mbali mbali vya siasa kikiwemo chama cha
mapinduzi (CCM) kujiunga na Chadema na kuchukua fomu za kuwania
nafasi hiyo ya ubunge jimbo la Kalenga.
Nyondo
alisema mwitikio huo ulioonyeshwa na wana Chadema jimbo la Kalenga
katika kujitokeza kuchukua fomu
ni mwanzo mzuri kwa Chadema kumrithi mbunge Dr Mgimwa jimbo hilo
la Kalenga na kuwaomba wana Kalenga kujitokeza kwa wingi
kumchangua mgombea wa Chadema mara katika uchaguzi mdogo wa
ubunge jimbo hilo utakaofanyika hivi karibuni .
katibu
huyo alisema kuwa hadi sasa maandalizi yote kwa ajili ya mkutano
maalum wa kura za maoni kwa wana Chadema kwa ajili ya kumteua
mgombea yamekamilika na (leo)
jumatano zoezi hilo litafanyika kwa wagombea waliojitokeza
kupigiwa kura za maoni.
Aliwataja
waliojitokeza kuomba kugombea nafasi hiyo kuwa ni pamoja na Zubery
Mwachura , Dr Evaristo Mtitu,Akbar Sanga, Grace Tendega, Rehema Makoga,
Sinkala Mwenda, Henry Kavina, Aidan Pungili, MUssa Mdede, Mchungaji
Samweli Nyakunga, Daniel *Luvanga,Anicent Sambala na Vitus Lawa .
Kwa
upande wake Aidan alisema kuwa anaingia katika mchakato huo kama
haki yake ya kidemokrasia pia kutaka kuwatumikia wana kalenga
ambao siku zote wamekuwa wakikosa kijana wa kuwatumikia zaidi ya
kuwapa wazee ambao wamekuwa hawawasaidii ipasavyo.
Pia alisema wana
kalenga wanapaswa kuachana na CCM na badala yake kuelekeza nguvu
zao kwa Chadema ambacho ni chama pekee kinachoweza kuwakomboa wana
kalenga.
Hata
hivyo mvutano mkubwa upo kwa wagombea hao ambao karibu wote
wanaonyesha kuwa na mvuto zaidi kwa wananchi kutokana na umaarufu
walionao katika jimbo hilo la kalenga .
Katika
wagombea hao zaidi ya wagombea watatu walipata kugombea ubunge
katika jimbo hilo kupitia CCM na Jahaz Asilia hivyo kuwa na majina
makubwa kwa wana kalenga wagombea ambao ni makada wa CCM ambao
walipohamia Chadema walikifanya chama hicho kupata pigo kubwa ni
pamoja na Mwachura ambae alipata kugombea ubunge jimbo la Iringa mjini
mwaka 2010 pamoja na akina Frederick Mwakalebela na kuamua kuondoka
CCM baada ya kuchakachua jina la Mwakalebela , pia Ansent Sambala
alipata kuomba kuwania
ubunge jimbo la Kalenga kupitia CCM kwa zaidi ya mara moja kabla ya
kuhamia Chadema pamoja na Grace Tendega ambae pia alipata kugombea
ubunge kupitia Jahaz Asilia katika jimbo hilo
Mwisho
0 comments:
Post a Comment