Thursday, 23 January 2014

UPINZANI UKRAINE,WATOA ONYO KWA SERIKALI

llllllll_51c99.jpg
Waandamanaji wakipambana na polisi mjini Kiev
Vifo hivyo ni vya kwanza tangu kuzuka kwa maandamano ya kuipinga serikali miezi miwili iliyopita. Waandamanaji na polisi nchini Ukraine wamepambana tena mapema leo (23.01.2014), baada ya ghasia kuzuka hapo jana Jumatano na kuigeuza sehemu ya katikati ya mji mkuu, Kiev kuwa uwanja wa vita, huku polisi wakitumia mabomu ya kutoa machozi na risasi za mpira dhidi ya waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe.
Vifo hivyo vimezusha hofu mpya baada ya miezi miwili ya maandamano ya kuipinga serikali yaliyochochewa na hatua ya serikali kutosaini makubaliano ya ushirikiano wa kibiashara na Umoja wa Ulaya, kutokana na shinikizo la Urusi.CHANZO DWSWAHILI

0 comments: