Monday, 6 January 2014

NAHODHA WA MVKILIMANJARO II ASEMA HAKUNA ALIYEANGUKA NUNGWI

NA 4606053 4835229 7842763 
Taarifa zilizochapishwa kwenye ZanziNews.com jioni hii zinasema kuwa juhudi za wananchi na vyombo husika mpaka sasa zimefanikiwa kuwapata wananchi wanne wakiwa hai na miili ya watu watano walioaga dunia (wanawake wawili na wanaume watatu). Miili ya maiti imehifadhiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja. Serikali itaandaa utaratibu wa kawaida kwa maiti kuzikwa ama kupewa jamaa zao. Kapteni Nassor Abubakar Khamis ameshikiliwa na jeshi la Polisi kwa mahojiano.  Zoezi la uokozi limesitishwa katika eneo la ajali kutokana na giza hadi hapo kesho asubuhi.


Kutokana na kuwepo kwa taarifa za kukanganya ambapo baadhi ya abiria wanadai kutokuwaona ndugu zao 7 kwa kuwa walianguka kwenye maji baada ya MV Kilimanjaro kukumbwa na dhoruba na hadi sasa hawajaonekana; Huku nahodha wa boti hiyo akikaririwa kusema kuwa hakuna yeyote aliyeanguka ama kuachwa
katika eneo la mkondo wa maji wa Nungwi; Wakati kamishna wa polisi Zanzibar Hamdan Makame amesema zipo ripoti ambazo hazijathibitishwa kuhusu watu 4 waliolazwa katika kituo cha afya cha Nungwi baada ya kuokolewa;
Blog ya Zanzibar Islamic News inaripoti kuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Rashid Seif Suleiman amsesema tayari kundi la wazamiaji tayari limekwenda katika eneo la ajali. Waziri Seif amesema kamati ya ulinzi na usalama imekutana mchana huu na kujadili tukio hilo kabla ya kuelekea eneo la tukio kushirikiana na wataalam wengine kuwatafuta watu hao.
Nalo Jeshi la polisi Zanzibar kwa kushirikiana na Jeshi la polisi Makao makuu Dar es salaam wametuma helkopta katika eneo la tukio ili kubaini watu ambao wanadaiwa kuzama katika eneo hilo.
Mkurugenzi wa Usafiri wa Baharini (ZMA) Mhandisi Abdi Maalim amesema mabaharia walianza kazi ya kuwatafuta watu wanaosadikiwa kuzama  majira ya alasiri leo  kwa kushirikiana na mabaharia wa kujitolea.
Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi Makosa ya Jinai Zanzibar DCI Yussuf Ilembo amesema uhakiki wa majina ya wahanga bado unaendelea ili kupata majina yao na umri wao kwa vile kuna meli mbili zilisafiri kwa wakati mmoja.




Taarifa zilizotolewa mchana wa leo kupitia vyombo mbalimbali vya habari zilisema kuwa mnamo wa majira ya saa tano adhuhuri ya leo, boti ya MV Kilimanjaro II mali ya kampuni ya Azam Marine, ilipatwa na dhoruba katika eneo la Nungwi wakati ikitokea Pemba kuelekea Unguja na kwamba abiria wapatao kumi hivi walianguka majini na kutupiwa maboya ya kujiokoa.Msemaji wa Polisi Zanzibar amekiri kutokea kwa dhoruba hiyo iliyosababishwa na upepo mkali ulioipiga boti hiyo iliyokuwa na abiria 369, watoto 60 na mabaharia 8 na kisha baadhi ya abiria kutupa maboya matano baharini bila ya maelekezo kutoka kwa nahodha wala mabaharia wa boti hiyo.  Lakini msemaji huyo amekaririwa akitamka kuwa kwa mujibu wa nahodha Aboubakar wa chombo hicho, hakuna mtu yeyote aliyedondoka ama kuachwa katika eneo la dhoruba na boti ilifanikiwa kutua nanga salama u salmin katika bandari ya Zanzibar mwendo wa saa sita kasoro mchana.

Related Posts:

0 comments: