Wednesday, 15 January 2014

AJALI YA PIKIPIKI YAUA MMOJA YAJERUHI IRINGA

Askari  wa  usalama  barabarani  katika  wilaya ya  Iringa ambae jina lake halikuweza  kufahamika mara moja  akiwa amemsimamisha mwendesha  pikipiki aliyepakia abiria (Mishikaki) kinyume na sheria.............................................................................. 

NA DIANA BISANGAO WA MATUKIO DAIMA.COM
IRINGA
MTU  mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa baada ya pikipiki walizokuwa wakiendesha kugongana maeneo ya Ipambasilo kijiji cha Ikuvala kata ya Isele tarafa ya Mazombe barabara ya Ilula- Uhambingeto wilaya ya Kilolo.
 
Imedaiwa marehemu huyo aliyetambulika kwa jina NICOLUS MGATA (15) alikuwa akiendesha pikipiki aina ya sunlg yenye namba za usajili T.733 BUE aligongana uso kwa uso na pikipiki aina ya sunlg yenye namba za usajili T.819 CHJ iliyokuwa ikiendeshwa na JUSTINE CHEWELE (20) mkazi wa ilula.
 
Akizungumza na mtandao  wa www.matukiodaima.com kamanda wa polisi mkoa wa Iringa RAMADHANI MUNGI alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea tarehe 13 januari mwaka huu.
 
Hata hivyo alisema marehemu alifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa hospitali ya teule ya itunda huku dereva wa pikipiki bwana CHEWELE amelazwa hospitali ya mkoa baada ya kuvunjika mguu. Kamanda MUNGI alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi.
 
Wakati huo huo jeshi la polisi mkoani Iringa linamshimkilia mtuhumiwa mmoja jina VEDASTO NGODA (28) Mkazi wa masege kwa kosa la kukutwa na kipande cha jino la tembo pamija na jino la kiboko katika gari lake.
 
Kamanda MUNGI alisema tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 14 januari  mwaka huu majira ya saa 2:30 usiku maeneo ya samora kata ya mshindo manispaa ya Iringa ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota mark II lenye namba za usajili T.793 ACP, alikutwa na vipande hivyo akiwa amevificha chini ya mito ya kukalia.
 
Aidha kamanda MUNGI alisema mbali na matukio hayo mawili tofauti, watu wasiofahamika waliibapikipiki aina ya fecon yenye namba za usajili T.389 CNG mali ya WAZIRI MSUMBWA(28) ni mfanyabiashara na mkazi wa mwangata manispaa ya Iringa iliyokuwa ikiendeshwa na SIJALI IDD (25) mkazi wa mlandege.
Dereva wa pikipiki amekamatwa kwa  mahojiano.
 

Related Posts:

0 comments: