Saturday, 15 February 2014

YANGA SASA RASMI KUIVAA AL AHLY BAADAYA KUICHAPA KOMOROZINE DE DOMONI 5-2

DSC_0051
Mabingwa wa Tanzania bara na wawakilishi wa nchi katika michuano ya kombe la mabingwa wa Afrika Dar Young African imefanikiwa kuvuka kwenda raundi ya pili ya michuano hiyo baada ya kuifunga timu ya Komorozine De Domoni mabao 5-2.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Mrisho Ngassa aliyefunga hat trick, huku Hamis Kiiza na Msuva wakifunga bao moja moja.
Yanga sasa watakutana na timu kubwa ya Misri Naciona Al Ahly.

  >>NGASSA APIGA HETITRIKI!

Kwenye Mechi ya Marudiano ya Raundi ya Awali ya Michuano ya CAF ya CHAMPIONZ LIGI iliyochezwa Leo huko Uwanja wa Sheikh Said Mohamed International, Mitsamihuli, Visiwa vya Comoro, Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga, wameitandika Komorozine de Domoni Bao 5-2 na kutinga Raundi ya Kwanza kwa Jumla ya Bao 12-2.
Wiki iliyopita Jijini Dar es Salaam, Yanga iliichapa Komorozine de Domoni Bao 7-0.
Katika Mechi ya Leo, Bao za Yanga zilifungwa na Hamis Kiiza, Dakika ya 13, Simon Msuva, Dakika ya 37, na Bao 3 za Mrisho Ngassa, kwenye Dakika za 22, 87 na 90.
Yanga sasa imesonga Raundi ya Kwanza ya CAF CHAMPIONZ LIGI ambapo watakutana na Mabingwa Watetezi, Al Ahly ya Misri, kati ya Februari 28 na Machi 2 na Marudiano kuchezwa kati ya Machi 7 na 9.
KIKOSI CHA YANGA:
Deogratias Munish "Dida", Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub "Cannavaro", Kelvin Yondani, Athuman Idd "Chuji", Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, Mrisho Ngasa, Hamis Kizza
Akiba: Barthez, Juma Abdul,Luhende, Rajab, Domayo, Dilunga n Bahanuzi
CAF CHAMPIONZ LIGI
RATIBA/MATOKEO:
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi za Kwanza au Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Jumamosi Februari 15
OS Balantas - Guinea-Bissau vs Sewe Sport - Ivory Coast
Steve Biko - Gambia  vs Entente Sportive de Sétif – Algeria [0-6, Biko wamejitoa]
Côte d'Or – Seychelles vs Kabuscorp – Angola [1-5]
Komorozine – Comoros 2   Young Africans – Tanzania 5 [2-12]
Kampala City Council FC – Uganda 1 El Merreikh – Sudan 2 [3-2]
Nkana FC – Zambia vs Mbabane Swallows – Swaziland [0-2]
Flambeau de l’Est – Burundi vs Diables Noirs – Congo [1-0]
Rayon Sports – Rwanda vs AC Leopards de Dolisie – Congo [0-0]
Black Africa – Namibia vs Kaizer Chiefs - South Africa [0-3]
Diamond Stars - Sierra Leone vs Raja Club Athletic – Morocco [0-6]
18:00 ASFA-Yennenga - Burkina Faso vs Diambars – Senegal [0-1]
Kano Pillars FC – Nigeria vs AS Vita Club - Congo, DR [1-3]
Bamako – Mali vs FAR Rabat – Morocco [2-2]
Jumapili Februari 16
Cnaps Sports – Madagascar vs Liga Muculmana de Maputo – Mozambique [0-1]
Mochudi Centre Chiefs – Botswana vs Dynamos – Zimbabwe [0-3]
Lioli – Lesotho vs Primeiro de Agosto – Angola [0-2]
Akonangui - Equatorial Guinea vs Les Astres de Douala - Cameroon [0-0]
Union Sportive Bitam – Gabon vs Gor Mahia – Kenya [0-1]
Foullah Edifice – Chad vs Al Ahli - Benghazi – Libya [0-4]
Douanes Niamey – Niger vs Al Zamalek – Egypt [0-2]
Anges de Notsè – Togo vs Enyimba International FC – Nigeria [1-3]
KMKM Zanzibar - Tanzania vs Dedebit – Ethiopia [0-3]
Barrack Y.C.II – Liberia vs  Asante Kotoko – Ghana [1-2]
Atlabara - South Sudan vs  Berekum Chelsea – Ghana [0-2]
Horoya Athlétique Club – Guinea vs F.C. Nouadhibou – Mauritania [1-1]
Stade Malien de Bamako – Mali vs USM EL HARRACH – Algeria [2-3]

Related Posts:

0 comments: