Tuesday, 18 February 2014

WATEULIWA WA CHADEMA NA CCM WARUDISHA FOMU




ccm_1_056ed.jpg
Mgombea wa nafasi ya ubunge katika jimbo la Kalenga kupitia CCM; Bw. Godfrey Mgimwa alipokuwa anatoka baada ya kukamilisha zoezi lake la kurudisha fomu hiyo.
chadema_4_4302c.jpg
Mgombea wa nafasi ya ubunge katika jimbo la Kalenga kupitia CHADEMA; Bi Grace Tendega alipokuwa anatoka baada ya kukamilisha zoezi lake la kurudisha fomu hiyo ya ugombea. 
Na Riziki Mashaka.
WAGOMBEA WA NAFASI YA UBUNGE KATIKA JIMBO LA KALENGA KUTOKEA VYAMA VYA CCM NA CHADEMA WALIPOKUWA WANARUDISHA FOMU HIZO LEO KATIKA UKUMBI WA SIASA NI KILIMO KATIKA ENEO HILO LA MANISPAA YA IRINGA, MWAKILISHI WA CCM NI GODFREY WILLIUM MGIMWA NA KUPITIA CHADEMA NI GRACE TENDEGA AMBAO WOTE WATAANZA KAMPENI ZAO SIKU YA KESHO YA TAREHE 19/02/2014.

Grace Tendega Mvanda  akirudisha fomu kwa Msimamizi wa Uchaguzi Pudenciana Kisika



Hapa akikabidhi fomu yake  kwa Msimamizi wa Uchaguzi, Pudenciana  Kisika
Mgombea wa CCM, Godfrey Mgimwa wa pili kushoto akiwa ameshika bendera ya CCM akielekea kurudisha  fomu 

Wana CCm wakimsindikiza  Mgombea  ubunge wa CCM Kalenga Bw Mgimwa kurejesha  fomu  leo 

Makada  wa Chadema  wakimsindikiza  mgombea  wao jimbo la kalenga leo 

msafara wa mgombea  ubunge  jimbo la kalenga kupitia  Chadema 


MGOMBEA  wa chama  cha mapinduzi (CCM) Godfrey Mgimwa na mgombea wa Chama cha  Demokrasia na maendeleo (Chadema) Grace T Mvanda Godfrey  Mgimwa wamerudisha fomu ya kugombea ubunge wa jimbo la Kalenga leo.

Wagombea hao   wamerudisha  fomu  hizo leo majira ya mchana ambapo mgombea  wa Chadema Grace T Mvanda  ndie alikuwa  wa kwanza  kurejesha akifuatiwa na mgombea wa CCM Bw Mgimwa 
Matukio yote  hayo  yalifanyika ndani ya ukumbi wa Siasa ni kilimo uliopo Gangilonga ambapo Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi Godfrey Mgimwa akisindikizwa na wanachama wa CCM alikabidhi fomu ya kugombea ubunge kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Iringa Vijijini Bi Prudenciana Kisaka.
Baada ya kurudisha fomu Godfrey aliwashukuru wananchi wa Kalenga na wanachama wa CCM kwa kumteua kuwa mgombea katika chama cha mapinduzi ccm na kuwaomba wananchi wawe watulivu siku ya uchaguzi na kuwaahidi kuwa uchaguzi wa Kalenga utakuwa wa amani.
Na kwa upande wa Katibu wa ccm mkoa wa Iringa Amina Imbo alisema kampeni zitaanza tarehe 19 februari mpaka tarehe 16 machi ambapo ndo itakuwa siku ya uchaguzi wa Mbunge wa Kalenga hivyo amewaomba wananchi kukipa kura chama cha mapinduzi pia amewasihi waandishi wa habari kuandika habari za haki na zenye ukweli na kuleta amani.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Iringa Vijijini Bi Delfina M. Mtavilalo amewashukuru wananchi wa Kalenga na wanachama wa chama cha mapinduzi kwa kuonyesha ushirikiano wao katika chama na kuwasihi wasishawishike kwa kuleta vurugu siku ya uchaguzi bali wapige kura kwa amani na kumchagua mbunge atakayeikwakilisha vizuri jimbo la kalenga.

Huku  mgombea  wa  Chadema Bi Mvanda  akiwahakikishia  wanachama  wa Chadema na wananchi wa jimbo la Kalenga  kuwa iwapo  atashinda katika nafasi  hiyo atahakikisha anafanya kazi ya kuwatumikia  wana Kalenga na  sio  kutafuta heshima  ya  uongozi.

Kwani alisema  kuwa ana uzoefu mkubwa katika kuongoza na  kuwa matatizo ya  jimbo la kalenga anayatambua   vema  hivyo atahakikisha  anatatua kero ya maji , umeme   na kilimo 

Related Posts:

0 comments: