Semina ya mafunzo ya msimamizi mkuu na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo na kata ya Kalenga imefunguliwa leo katika ukumbi wa Siasa ni kilimo katika Manispaa ya Iringa huku mgeni rasmi akiwa ni Mkuu wa wilaya ya Iringa Dokta Leticia Warioba.
Akiongea
mbele ya washiriki wa Semina hiyo Dokta Warioba alisema uchaguzi unakaribia
kufanyika hivi karibuni hivyo amewataka wawe waaminifu na makini siku ya
uchaguzi pia hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakaekiuka sheria
na taratibu za usimamizi wa uchaguzi.
Na
kwa upande wa Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kalenga ambaye pia ni mkurugenzi
mtendaji wa wilaya ya Iringa Prudencia Kisaka aliitaja siku ya kutoa fomu za
uteuzi ni kuanzia tarehe 9 mpaka tarehe 18 mwezi huu.
Pia
amesema uteuzi wa vyama utaanza tarehe 18 mwezi huu ambapo kampeni za wagombea
zitafanyika tarehe 19 februari mpaka tarehe 15 machi mwaka huu, hivyo siku ya
upigaji kula itakuwa ni tarehe 16 machi ambapo daftari litakalotumika ni lilelile
la mwaka 2010.
NA
DIANA BISANGAO WA , IRINGA
0 comments:
Post a Comment