Wednesday, 5 February 2014

RUMMENIGGE AITAKA UEFA IWASHUGHULIKIE PSG KUVUNJA FFP!

>>ENGLAND KUIPINGA MAN CITY YAFUKUTA!!
Karl-Heinz_RummeniggeMWENYEKITI wa Mabingwa wa Ulaya Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge, ameitaka UEFA ichukue hatua dhidi ya Paris St Germain ikiwa Klabu hiyo imevunja Kanuni mpya za chombo hicho, Uchezaji Haki Kifedha, Financial Fair Play, FFP.
Kanuni za FFP zimeanza kutumika Msimu huu baada kuwa na Kipindi cha Mpito cha Miaka Mitatu na, kimsingi, zinataka Klabu zisitumie Fedha zaidi ya Mapato yao yanayotokana na Haki za TV, Tiketi Milangoni, Udhamini na Zawadi za Ushindi kwenye Mashindano.IBRAHIMOVIC_with_PSG
Ingawa Mfumo huo unaruhusu Madeni kwa kiwango fulani lakini upo mahsusi kuzuia Matumizi mabovu ya Klabu kwenye Mishahara ya Wachezaji na Uhamisho wao wakitegemea Ruzuku toka kwa Wamiliki wao Matajiri.
Akiituhumu PSG, Rummenigge, ambae mbali ya kuwa Mwenyekiti wa Bayern Munich pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Vilabu huko Ulaya, European Club Association, amesema: “Sifikirii kama Paris St Germain wanafuata FFP. Sote tunajua Fedha zinazotiririka toka kwa Wamiliki wao, inadaiwa ni Euro Milioni 200 kwa Msimu. Natumai Rais wa UEFA, Platini, atafuatilia. Klabu zinazovunja FFP zichukuliwe hatua. Haiwezekani CHAMPIONZ LIGI iamuliwe na Matajiri toka Urusi au Arabuni! ”
PSG ilinunuliwa na Wawekezaji kutoka Qatar Mwaka 2011 na kutumia Fedha nyingi kuwanunua Wachezaji wakubwa kama vile Zlatan Ibrahimovic, Edinson Cavani na Thiago Silva na Msimu uliopita walitwaa Ubingwa wa France kwa mara ya kwanza tangu 1994.
Msimu huu wako Pointi 5 mbele kileleni mwa Ligi 1 na wapo kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ambapo watakutana na Bayer Leverkusen baadae Mwezi huu.
Huko England kuna minong’ono wapo Wanasheria wa Vilabu kadhaa ambao wana tafakari kupinga Manchester City kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu ujao wakitaka Mahesabu yao yachunguzwe kwa sababu hawaamini kama yanakidhi FFP.
Kitu hiki pia kilidokezwa na Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho, Siku kadhaa zilizopita.

Related Posts:

0 comments: