Saturday, 8 February 2014

NORWICH CITY YAMTOA JASHO MANCHESTER CITY YAMKOSESHA KUONGOZA LIGI(0-0)

MAN C
Manchester City katika 180 bila goli hata moja.
Timu ya Pellegrini Man City, baada ya kushindwa goli moja kwa bila nyumbani na timu ya Chelsea Jumatatu iliyopita; Jumamosi hii ilikumbana na tatizo kubwa la kutoweza kuingiza goli hata moja katika nyavu za Norwich.
Norwich City iliyokuwa imefungwa magoli saba na Man City katika mechi ya kwanza, Jumamosi hii waliweka ukuta mkubwa na kufunga milango yao ili City wasiwaingize goli. Kwa hiyo timu hizi zikatoka sare.
Matarajio yake Pellegrini ya kukalia nafasi ya kwanza yameisha wikendi hii kwa kuwa wamepinduliwa na klabu ya Chelsea baada ya kuilaza Newcastle magoli matatu kwa nunge.

Takwimu ya mchezo:
Norwich (4-2-3-1): Ruddy; Martin, Yobo, Bassong, Olsson; Tettey, Johnson, Pilkington (Whittaker 90), Fer, Redmond, Hooper (Van Wolfswinkel 68,).
Wasiotumiwa: Bunn, Hoolahan, Garrido, Becchio, Murphy.
Kadi za manjano: Tettey, Van Wolfswinkel.
Kocha: Chris Hughton
Manchester City (4-4-2): Hart; Zabaleta, Kompany, Demichelis, Clichy, Navas, Milner, Toure, Silva, Jovetic (Dzeko 61), Negredo (Kolarov 77).
Wasiotumiwa: Pantilimon, Richards, Lescott, Rodwell, Lopes.
Kadi ya manjano: Milner.
Kocha: Manuel Pellegrini
Mchezaji hodari: Fer
Refarii: Jon Moss
Mahudhurio: 26,832.

Related Posts:

0 comments: