Tuesday, 11 February 2014

MOURINHO ASHUSHUKA! YAYA TOURE APONA RUNGU LA FA!

KIUNGO wa Manchester City Yaya Toure hatachukuliwa hatua yeyote ya Kinidhamu kwa kosa la kumpiga teke Mchezaji wa Norwich City, Ricky van Wolfswinkel, wakati Timu zao zilipotoka Sare 0-0 hapu Jumamosi huko Carrow Road.
FA imethibitisha kuwa Toure hana Kesi ya kujibu baada ya Jopo Huru la Marefa Watatu wa zamani kulipitia tukio hilo na kushindwa kuafikiana kwa kauli moja kuwa Toure alipaswa kupewa Kadi Nyekundu.
Ili FA imfungulie Mashitaka Mchezaji inabidi Jopo hilo limekubaliane wote kwa pamoja.
HABARI ZA AWALI:

MOURINHO ATAKA YAYA TOURE AFUNGIWE!!
>>AKIFUNGIWA KUIKOSA CHELSEA JUMAMOSI!
BOSI wa Chelsea Jose Mourinho amesema Mchezaji wa Manchester City, Yaya Toure, anastahili kufungiwa kwaMOURINHO-CHELSEA_TRAINING kumpiga teke Mchezaji wa Norwich City, Ricky van Wolfswinkel.
Toure, mwenye Miaka 30, anaweza kufungiwa Mechi 3 kwa tukio hilo liliotokea huko Carrow Road Jumamosi iliyopita wakati Man City ilipobanwa na kutoka Sare 0-0 na Norwich City.
Akizungumzia tukio hilo, Mourinho amesema: “Kama hafungiwi basi ujumbe ni wazi: unaweza kufanya lolote. Kama FA inatetea Soka, basi lazima afungiwe.”
Ikiwa atafungiwa, basi moja ya Mechi ambazo Toure atazikosa ni ile ya Jumamosi wakati Man City itakapopambana na Chelsea kwenye Raundi ya Tano ya FA CUP huko Etihad.
FA imesema inangoja Ripoti ya Refa Jon Moss ili itafakari nini cha kufanya.
Akiongelea tukio hilo ambalo Marefa hawakuliona, Meneja wa Norwich City, Chris Hughton, amekiri: “Hakika kulikuwa na kitu lakini kama ni Kadi Nyekundu hiyo ni juu ya Refa kuamua!”
FA CUP
Raundi ya Tano
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumamosi Februari 15
1545 Sunderland v Southampton
1800 Cardiff v Wigan
1800 Sheff Wed v Charlton
2015 Man City v Chelsea
Jumapili Februari 16
1630 Everton v Swansea
1800 Sheff Utd v Nottm Forest
1900 Arsenal v Liverpool
Jumatatu Februari 17
2245 Brighton v Hull

Related Posts:

0 comments: