Monday, 3 February 2014

MAZISHI YA AFANDE JEMA J. LUVINGA MKOANI IRINGA




Mkuu wa Polisi Mkoa wa Iringa Kamanda Ramadhan Mungi akitoa nasaha kama sehemu ya salaam za rambirambi Polisi mkoa wa Iringa. Katika salaam hizo mkuu huyo wa mkoa amesema jamii inao wajibu kushirikiana na jeshi la polisi katika kupunguza ajali hizo. Ameelezwa kusikitishwa na baadhi ya abilia kushiriki kumchochea deleva aende mwendo wa kasi ambao mara nyingi umekuwa ni chanzo kikubwa cha ajali. Amesisitiza kwamba jeshi la polisi mkoani Iringa litaongeza juhudi zake katika kupunguza ajali. Akikazia jambo hili Kamanda Mungi alisema “… Leo tumejumuika nanyi kwa tukio maalumu la kumpoteza askari mwenzetu kwa kifo kilichosababishwa na ajali usiku wa tarehe 31/01/2014…tumepoteza askari mdogo sana tuliyemtegemea. Tutakuwa wakali zaidi katika hili kwa sababu taifa linapoteza sana watu wake kwa njia ya ajali”


Kamanda Mungi akiwa na waombolezaje wengine….

Mwakilishi wa Mkuu wa chuo cha mafunzo ya Polisi Moshi Assistant Inspector Castory Chali alitoa nasaha mara tu baada ya salaam za RPC wa Iringa.  


Viongozi zaidi wa polisi…


Sehemu ya waombolezaji.

Related Posts:

0 comments: