Monday, 3 February 2014

KOMBE LA DUNIA:BAA/PUB KUA WAZI USIKU WA MANANE ENGLAND IKICHEZA!

>>WAZIRI MKUU UINGEREZA AINGILIA KATI ILI BAA ZIWE WAZI!
WAZIRI MKUU wa Uingereza, David Cameron, ametaka ifikiriwe upya ili kuruhusu Mabaa kubakiENGLAND_IN_WEMBLEY wazi Usiku wa Manane ili kuruhusu Watu kutazama Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa huko Brazil kuanzia Juni 12 baada ya Mawaziri kupinga Mabaa hayo kuwa wazi kwa Mechi za England.
Wamiliki Pabu hizo waliomba muda wao wa kuwa wazi uongezwe lakini Wizara ya Mambo ya Ndani ilipinga ombi hilo lakini sasa kuna taarifa toka Ofisi ya Waziri Mkuu kuwa ruhusa itatolewa. 

KOMBE LA DUNIA-BRAZIL 2014
England=Kundi D:
RATIBA:
-Juni 14: v Italy
-Juni 19: v Uruguay
-Juni 24: v Costa Rica
England, ambao wako Kundi C kwenye Fainali za Kombe la Dunia, wataanza Mechi zao Juni 14 kwa kucheza na Italy Saa 5 Usiku kwa Saa za Uingereza, ikiwa ni Saa 7 Usiku Saa za Bongo.
Katika Mechi zao nyingine mbili za Kundi C, England watacheza na Uruguay kuanzia Saa 2 Usiku kwa Saa za Uingereza, ikiwa ni Saa 4 Usiku Saa za Bongo na kufuatia Costa Rica watakayocheza Saa 11 Jioni, Saa za Uingereza, ambayo ni Saa 1 Usiku kwa Bongo.
Kwenye Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2010 zilizochezwa huko Afrika Kusini, zaidi ya Watu Milioni 4 waliitazama Mechi ya ufunguzi ya England wakiwa kwenye Pabu huko Uingereza.

Related Posts:

0 comments: