Monday, 17 February 2014

HOT NEWSSS MSAFARA WA MGOMBEA UBUNGE CHADEMA KALENGA WAZUIA NA POLISI IRINGA

Polisi Iringa wakiwa  wameuzua msafara  wa mgombea  ubunge jimbo la Kalenga  Bi Grace Tendega kupitia Chadema kwa madai  hawakuwa na kibali cha kufanya  maandamano  hayo ya magari  hapa  ni eneo la lango la mji Samora ambapo msafara huo  ulikuwa ukitokea maeneo la Ndiuka kuelekea kwa msimamizi wa uchaguzi  ili kuchukua fomu  ya NEC 
Mgombea  ubunge wa  Chadema kalenga Grace Tendega baada ya  kuruhusiwa  gari lake kupita 
Hapa  polisi  wakimtazama  mgombea  huyo akipita  mbele yao 
 

Diwani Nyalusi kati  akiwa  chini ya ulinzi wa  polisi 
Diwani wa Chadema kata ya Mvinjeni Iringa mjini Frank Nyalusi wa pili kushoto akiwa chini ya ulinzi  wa  polisi leo 
Viongozi  wa Chadema  Iringa wakiwa na mgombea  wa ubunge  jimbo la Kalenga katikati  Bi Grace  T Mvanga 
mgombea  wa  Chadema jimbo la Kalenga Grace T Mvanga akizungumza na wanahabari  leo baada ya  kuchukua fomu 
JESHI  la  polisi  mkoani  Iringa   leo   limeuzuia kwa muda msafara  wa  mgombea  ubunge jimbo la Kalenga  kupitia  chama  cha  Demokrasia na maendeleo (CHADEMA)  Grace Tendega Mvanga    kwa madai  kufanya  maandamano  yasiyo na  kibali.

Huku  Polisi  hao   wakimshikilia kwa  muda  diwani  wa  kata ya  Mivinjeni Frank Nyalusi ( Chadema) kwa madai ya  kuandaa mapokezi  hayo  bila kibali .

Tukio la  kuzuiwa kwa  mgombea  huyo  lilitokea  mida ya saa 5 asubuhi   wakati msafara wa  mgombea  huyo ukiwa na magari  zaidi ya matano na pikipiki zaidi ya 20 ukikaribia kuingia Samora  katika mji  wa Iringa .

Hata   hivyo  mbali ya msafara  huo  kuzuiwa zaidi ya dakika 20  katika eneo hilo Mlima  wa  Ipogolo  barabara  kuu ya  Iringa- Dodoma polisi  waliweza kutumia busara  zaidi ya kumruhusu  mgombea  wao kupita  kuelekea kuchukua  fomu  huku  wafuasi  wengine   wakizuiliwa kwa dakika tano  na  kuruhusiwa kumfuata mgombea  wao  ili  kuufanya msafara  huo kuwa katika  hali ya kawaida na sio maandamano kama  ilivyokuwa awali.

Pamoja na  kuwaruhusu  wafuasi hao ambao  baadhi yao  walianza  kutoa lugha ya matusi kwa askari hao na  kuwalazimisha  kufyatua risasi jambo  ambalo  askari  hao  polisi  hawakuweza  kufanya  hivyo  wala  kuwapiga mabomu ya machozi  zaidi ya  kumchukua kiongozi  wao Frank Nyalusi kwa mahojiano  zaidi.

Akizungumzia  hatua  ya polisi  kuzuia msafara  huo kwa  muda  katibu  wa Chadema  wilaya ya  Iringa  vijijini Felix Nyondo  alisema  kuwa   wameshangazwa na hatua ya polisi  kuzuia msafara  huo kwani  hayo hayakuwa maaandamano bali ni mgombea  wao kutoka nyumbani kwenda kuchukua fomu kwa mujibu  wa  utaratibu wa msimamizi wa uchaguzi  huo.

Nyondo  alisema  walivyofanya  Chadema ni kama  walivyofanya CCM  wakati mgombea  wao akienda kuchukua fomu ambapo CCM  walikwenda mbali  zaidi kwa  kuwa na  watu ambao  walikuwa  wakitembea kwa  miguu na  wao Chadema   hawakufanya  hivyo  na badala  yake  walitumia magari na pikipiki kuelekea kwa msimamizi  huyo.

Kamanda  wa  polisi  mkoa  wa Iringa Ramadhan Mungi alipotafutwa kwa  njia ya  simu na mtandao huu wa www.matukiodaima.com  ili  kuelezea  zaidi hatua ya  kuzuia msafara  huo na kumshikilia kada  huyo wa Chadema hakuweza kupatikana japo  mmoja kati ya maofisa wa  polisi  waliokuwepo  eneo la  tukio alisikika akisema  kuwa  lengo la  kuzuia msafara  huo halikuwa lina ubaya ila ni katika polisi kutimiza wajibu  wake wa  kuhakikisha kila kitu  kinafanyika kwa  misingi ya  sheria.

Kwani  alisema Chadema  walipaswa  kuomba kibali kwa ajili ya  kumpokea na  kumsindikiza  mgombea  wao kuchukua fumu   na polisi wangekuwepo kwa ajili ya kulinda  usalama  wao ikiwa ni  pamoja na kuwaongoza  njia ambavyo  wangependa  kupita  ila  sio hivyo walivyofanya  kwa  kutumia nguvu kusababisha msongamano  wa magari  katika  barabara  hiyo.

Kwa  upande  wake mgombea   ubunge wa  Chadema kalenga Bi Mvanga  akizungumza na  wanahabari  alisema kuwa anawapongeza wana Chadema  jimbo la kalenga  kwa  kuendelea  kumuunga mkono na  kuwa   lengo  la Chadema ni kuona  wana Kalenga  wanampata  mrithi wa  aliyekuwa mbunge wa  jimbo hilo marehemu  Dr Wiliam Mgimwa (CCM) mwenye  uwezo  wa  kuwatumikia  wananchi ambapo kwa upande  wake anao uwezo  huo.

Mgombea  huyo  alipongeza  shughuli mbali mbali  za kimaendeleo  zilizofanywa na mbunge Dr Mgimwa kwa jimbo la kalenga  na  kuahidi  kuendeleza jitihada  hizo za kimaendeleo  iwapo  wananchi  wa Kalenga  watamchagua  katika  uchaguzi  huo mdogo.

" Kuna mambo ambayo marehemu  aliahidi na  kuishia njiani katika  kuyafanikisha na  kuwa nafasi  hiyo  ataitumia kwa  kufuatilia  yote ambayo hayajafikia  ukingoni "

Kuhusu  msafara  wake kuzuiwa na  polisi alisema  kuwa  hizo ni changamoto  za  kuwaida katika  kuelekea  kwenye  ukombozi  wa kweli  kwa wana kalenga  kumpata kiongozi makini .

Zoezi la uchukuaji fomu la mgom bea huyo lilifanyika majira ya saa sita mchana katika ofisi za msimamizi wa uchaguzi Jimbo la KalengaPudenciana Kisaka ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halimashauri ya Iringa Vijijini.
 Kisaka alimkabidhi fumo namba 8 mgombea huyo pamoja na nyaraka mbalimbali za Tume ya uchaguzi ikiwamo sheria za uchaguzi Kanuni za uchaguzi na pia katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na kumtaka mgombea kwenda kujisomea kwa lengo la kuongeza uelewa ili kuepusha vurugu wakati wa kampeni na uchaguzi wenyewe.
 Kisaka aliwaambia waandishi wa habari kuwa hadi sasa ni wagombea wawili kutoka vyama vya CCM na Chadema pekee ndio wamejitokeza kuwania kiti cha Ubunge katika jimbo hilo huku akiongeza kuwa mwisho wa kurejesha fomu ni Februari 18 mwaka huu .
 “Hadi sasa tunavyama viwili ambavyo wagombea wake wameshachukua fomu ya kuwania Ubunge kwa jimbo la Kalenga ,hata hivyo sheria bado inatoa Fursa kwa vyama kuendelea kujitokeza hadi kuchukua na kurejesha hadi  leo kabla ya saa kumi jioni”alisema Kisaka.
 Uchaguzi wa Kalenga unatarajia kufanyika Machi 16 mwaka huu na unalengo la kuziba pengo lililoachwa wazi na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Marehemu Dk Wiliam Mfimwa aliyefariki dunia Januari Mosi mwaka huu,katika uchaguzi huo CCM imemsimamisha Godfrey Mgimwa mmoja w awatoto w marehemu Mgimwa kupeperusha bendara ya chama hicho.
 Grace  T Mvanga  alipata  kugombea  jimbo la Kalenga kwa mara ya kwanza  mwaka 2005 kupitia  Chama cha Jahazi Asilia na kushika nafasi ya  pili kwa  kura  13000 huku mgombea wa CCM  kwa  kipindi hicho George Mlawa  akishinda kwa  kishindo na bila kukata tamaa mwaka 2010 Grace  T.Mvanda  alijitokeza  tena  kugombea  kupitia chama cha Jahazi Asilia na kushuka kwa  kupata  kura 3000 pekee huku mgombea wa CCM Dr  Wiliam Mgimwa akiongoza na  safari  hii kuibukia  Chadema ambao  anagombea kwa mara ya kwanza kupitia Chadema na mara ya tatu katika Historia  yake ya  kuusaka ubunge Kalenga hivyo macho na masikio ya  wengi  kuona kama atapanda ama atazidi  kushuka zaidi 

Related Posts:

0 comments: