Mechi hii, maarufu huko Jijini Madrid
Nchini Spain kama El Derbi madrileño, ilikuwa pia na burudani tosha kwa
vitimbwi kati ya Sentahafu wa Real Kepler Laveran Pepe na Fowadi wa
Atletico Diego Costa wakifanyiana undava na kutishana huku, kama kawaida
yake, Sergio Ramos, akitia chapuo za hapa na pale.
Atletico, ambao ndio Mabingwa Watetezi
wa Kombe hili na pia ni Vinara wa La Liga wakiwa Pointi 3 mbele ya
Barcelona na Real zinazofungana kwa Pointi, walitinga kwenye Mechi hii
wakiwa na nia ya kujihami kwa kumwacha Diego Costa kuwa Straika pekee.
Real, ambao walitawala, walikuwa shapu
na kuonana sana, walipata Bao la kwanza Dakika ya 17 baada ya Shuti la
Pepe kumbabatiza Insua na kutinga.
Bao la Pili la Real, lilikuwa safi sana, kufuatia ushirikiano mzuri na Jese Rodriguez kumalizia kwenye Dakika ya 57.
Bao la Tatu ni la Shuti la Angel Di Maria ambalo lilimbabatiza Joao Miranda na kutingisha kamba kwenye Dakika ya 73.
Timu hizi zitarudiana huko Estadio
Vicente Calderon hapo Jumanne Februari 11 na ili Atletico waendelee
kulitetea Taji lao inabidi waichape Real Bao 4-0.
VIKOSI:
REAL MADRID [Mfumo: 4-3-2]:
-Casillas
-Arbeloa, Pepe, Ramos, Coentrao
-Modric, Alonso, Di Maria
-Jese, Benzema, Ronaldo
Akiba: Illarremendi, Morata, Marcelo, Lopez, Isco, Carvajal, Varane
ATLETICO MADRID [Mfumo: 4-2-3-1]:
-Courtois
-Juanfran, Miranda, Godin, Insua
-Koke, Gabi
-Garcia, Diego, Turan
-Diego Costa
Akiba: Manquillo, Rodriguez, Tiago, Sosa, Alderweireld, Adrian, Aranzubia
REFA: Clos Gómez
Barcelona v Real Sociedad
COPA del REY
NUSU FAINALI
[Saa za Bongo]
Marudiano
Jumanne Februari 11
23:00 Atletico de Madrid v Real Madrid CF [0-3] [Estadio Vicente Calderon]
Jumatano Februari 12
24:00 Real Sociedad v FC Barcelona [Estadio Anoeta]
FAINALI
Aprili 19
0 comments:
Post a Comment