Wednesday, 5 February 2014

WEST HAM YATISHIA KUTUA KORTINI KUPINGA KUFUNGIWA CARROLL!

>>WADAU WADAI ADHABU YA CARROLL NI KULINDA KOSA LA REFA WEBB!
ANDY_CARROLLWest Ham United imetishia kuchukua hatua za Kisheria dhidi ya FA ikiwa watakataa kumkubalia Straika wao Andy Carroll kupewa nafasi nyingine ya kujitetea baada ya Rufaa yake kupinga Kadi Nyekundu kutupwa nje na Jopo Huru la FA na hivyo kufungiwa Mechi 3.
Kwa mujibu wa Kanuni za FA, Chama cha Soka England, uamuzi wa Jopo Huru ni wa mwisho na hauwezi kukatiwa Rufaa nyingine.
West Ham inasemekana imeiandikia FA kutaka ombi lao litolewe jibu ifikapo Ijumaa na pia imesisitiza kuwa itapeleka suala hilo Mahakamani ikiwa watagomewa kitu ambacho hakijawahi kutokea England.
Wakisaidiwa na Mwanasheria mahiri huko Uingereza, QC Lord David Pannick, West Ham walituma Barua hiyo wakielezea kuhuzunishwa kwao na kesi hiyo ya kumwadhibu Andy Carroll na kumfungia Mechi 3 bila kujitetea.
Carroll alipewa Kadi hiyo Jumamosi wakati Timu yake inaichapa Swansea City Bao 2-0  na kuonekana na Refa Howard Webb kuwa alimpiga kipepsi Beki wa Swansea Chico Flores ingawa marudio ya tukio hilo yalionyesha Beki huyo hakupigwa bali aliparazwa na mkono wa Carroll juu ya kichwa waliporuka wote juu.
Kifungo hicho kitamfanya Andy Carroll azikose Mechi 3 muhimu za West Ham ambao wanapigania kukwepa kuburutwa kwenye vita ya kushuka Daraja.
Mechi ambazo atazikosa Carroll ni zile na Aston Villa, huko Villa Park Siku ya Jumamosi, na zile za Nyumbani Uwanjani Upton Park dhidi ya Norwich na Southampton.
Hata hivyo, FA imekataa kusema lolote kuhusu uamuzi huu wa West Ham.
Lakini Wadau wengi wa Soka huko England wanahisi Carroll ameonewa na ‘mwongo’ Chico Flores ndie aliepaswa kuadhibiwa zaidi.
Miongoni mwa walioibuka na kuiponda FA kwa uamuzi huu ni Meneja wa zamani Neil Warnock ambae sasa ni Mchambuzi wa Soka aliedai uamuzi huo wa FA ni kumlinda Refa Howard Webb kwa makosa yake kwa vile anaiwakilisha England kwenye Kombe la Dunia huko Brazil.

Related Posts:

0 comments: