Wednesday, 5 February 2014

CRISTIANO RONALDO AFUNGIWA MECHI 3!

RONALDO_IN_REALCRISTIANO RONALDO amefungiwa Mechi 3 lakini Leo hii atacheza Mechi ya Kwanza ya Nusu Fainali ya Copa del Rey dhidi ya Atletico Madrid Uwanjani Santiago Bernabeu
Chama cha Soka cha Spain, RFEF, kimempa Mchezaji huyo wa Real Madrid ambae pia ndio Mchezaji Bora Duniani Kifungo cha Mechi 3 kufuatia Kadi Nyekundu aliyopewa kwenye Mechi na Athletic Bilbao Jumapili iliyopita ambayo ilimalizika kwa Sare ya Bao 1-1.
Ronaldo, ambae Leo anasheherekea Miaka 29 tangu kuzaliwa, alipewa Kadi Nyekundu kwenye Dakika ya 76 baada kukwaana na Wachezaji wa Bilbao Ander Iturraspe na Carlos Gurpegui.
RFEF imempa Ronaldo Kifungo cha Mechi moja kufuatia Kadi Nyekundu na kumuongezea Mechi mbili kwa kutoa ishara iliyotafsiriwa kuwa ni kebehi kwa Marefa wakati akitoka nje mara baada ya Kadi hiyo.
Kifungo hiki cha Mechi tatu kinamaanisha atazikosa Mechi za Real Madrid za La Liga dhidi ya Villareal, Februari 9, na Elche, Februari 23, zote zitachezwa Uwanjani Santiago Bernabeu na ile ya Ugenini hapo Februari 16 na Getafe.
Licha ya Kifungo hiki, Ronaldo yuko huru kuichezea Real Mechi zote mbili za Nusu Fainali ya Copa del Rey dhidi ya Atletico Madrid ambayo ya Kwanza ni Leo na Marudiano ni Wiki ijayo.

Related Posts:

0 comments: