>>SASA NAFASI YA TEVEZ KWENDA BRAZIL FINYU!!
Kocha wa Argentina, Alejandro Sabella,
ameteua Kikosi chake cha Wachezaji 22 kuwavaa Romania hapo Machi 5 huko
Bucharest na kama ilivyo kawaida yake tangu awe Kocha wa Nchi hiyo Tevez
hakuitwa.
Msimu huu akiwa na Juventus, Carlos
ameshafunga Bao 14 na mara ya mwisho kuichezea Argentina ni kwenye Copa
America Mwaka 2011 wakati Kocha wa Argentina ni Sergio Batista.
Wachezaji wengine maarufu ambae
hawakuitwa ni Esteban Cambiasso, Kipa wa Malaga, Willy Caballero, na
Fowadi wa Tottenham, Erik Lamela.
Kikosini, kama ilivyotarajiwa na wengi, wamo Mafowadi hatari, Lionell Messi na Sergio Aguero.
Baada ya kucheza na Romania, Argentina
watacheza Mechi nyingine za Kirafiki dhidi ya Trinidad & Tobago na
Slovenia Mwezi Juni.
Kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil, Argentina wako Kundi F pamoja na Bosnia-Herzegovina, Iran na Nigeria.
KIKOSI KILICHOTEULIWA:
Makipa: Sergio Romero (Monaco), Mariano Andujar (Catania)
Mabeki: Pablo Zabaleta
(Manchester City), Federico Fernandez (Napoli), Ezequiel Garay
(Benfica), Marcos Rojo (Sporting Lisbon), Hugo Campagnaro (Inter), Jose
Basanta (Monterrey), Lisandro Lopez (Getafe), Nicolas Otamendi (Atletico
Mineiro), Gino Peruzzi (Catania)
Viungo: Javier
Mascherano (Barcelona), Angel Di Maria (Real Madrid), Lucas Biglia
(Lazio), Ricardo Alvarez (Inter), Augusto Fernandez (Celta Vigo), Jose
Sosa (Atletico Madrid)
Mafowadi: Lionel Messi
(Barcelona), Gonzalo Higuain (Napoli), Sergio Aguero (Manchester City),
Ezequiel Lavezzi (Paris Saint-Germain), Rodrigo Palacio (Inter).
0 comments:
Post a Comment