Thursday, 9 January 2014

WATU WAWILI WAFARIKI DUNIA MKOANI IRINGA KWA MATUKIO TOFAUTI


                          RPC Iringa Maramdhan Mungi
....................................................................................................................................................
Na DIANA BISANGAO, Matukiodaima.com Iringa

Watu wawili wafariki dunia mkoani Iringa katika matukio mawili tofauti likiwemo la mwanaume mmoja mkazi wa kijiji cha Nyamihuu mkoani Iringa kupata ajali ya trekta aliyokuwa akiendesha kuacha barabara na kupinduka.

Imedaiwa mwanaume huyo aliyetambulika kwa jina Herman Sanga (22) alikuwa akiendesha trekta lenye namba za usajili 6656 aina ya Fiat mali ya Kriakos Kalogeresi mkazi wa Iringa alikuwa akitokea shambani akielekea nyumbani ambapo trekta alilokuwa akiendesha liliacha barabara na kupinduka  na kusababisha majeruhi.

Akizungumza na wandishi wahabari ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea January 5.

Hata hivyo alisema kuwa majeruhi huyo alikimbizwa katika hospitali ya serikali Tosamaganga kwa matibabu zaidi ambapo majira ya saa mbili usiku alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu, Kamanda Mungi alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi.

Wakati huohuo Jeshi la polisi Mkoani Iringa linamshikiria mtuhumiwa mmoja aliyejulikana kwa jina la Denis Kamugisha  (34) kwa kosa la kumgonga mwendesha pikipiki ambaye jina lake halijafahamika na kusababisha kifo kwa abiria wake aitwaye Costantine Msuva mkazi wa boma la ng’ombe huku dereva wa pikipiki akiwa amelazwa na hawezi kuzungumza.

Kamanda Mungi alisema kuwa tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 5 january majira ya saa 9:50 alasiri maeneo ya Boma la Ng’ombe Kata ya Kidabaga Tarafa ya Kilolo Wilaya ya Kilolo ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa akiendesha gari aina ya land cruser lenye namba za usajiri T.222 APR alimgonga mwendesha pikipiki aina ya sky mark ambapo namba za usajiri hazijafahamika, chanzo cha ajali bado hakijafahamika.

Aidha Kamanda Mungi amesema mbali na matukio hayo mawili ya ajali tofautitofauti pia watu wasiofahamika waliiba ng’ombe kumi na tisa (19) wenye thamani ya shilingi milioni kumi na moja za kitanzania (11000000/=Tshs) mali ya Maganga Madagana (27) mkazi wa kijiji cha Mfyome, chanzo cha tukio hilo kinaeleza ni tama ya mali ambapo watuhumiwa wanatafutwa.

Related Posts:

0 comments: