SHABIKI ACHOMWA KISU ANFIELD!
Polisi wa Kitongoji cha Merseyside
walisema Mtu mmoja mwenye Umri wa Miaka 35 alisimamisha Ambulensi
iliyokuwa ikipita jirani na maeneo ya Uwanja wa Anfield mara baada ya
Mechi hiyo.
Hata hivyo Polisi wamesema Shabiki huyo aliechomwa Kisu ambae yuko salama amekataa kusema chochote kwa Polisi.
Polisi imewataka Mashahidi walioshuhudia tukio hilo wajitokeze kutoa Taarifa.
MOYES AHAKIKISHIWA FEDHA KUNUNUA WAPYA!
Meneja wa Manchester United David Moyes amehakikishiwa kuwa zipo Fedha za kununua
Wachezaji wakati huu wa Dirisha la Uhamisho la Januari na pia mwishoni mwa Msimu.
Inaaminika Klabu inalenga kumnunua
Fulbeki wa Kushoto na Kiungo mmoja lakini hawatahaha kununua Mchezaji
ili mradi kununua tu bali watalenga Wachezaji Bora wanaokidhi viwango
vyao.
Mara baada ya kufungwa hapo Jana Bao 2-1
na Swansea City na kutupwa nje ya FA CUP, David Moyes alikiri Timu
inahitaji nguvu mpya ya Wachezaji wapya lakini alisema: “Tunataka kuleta
Wachezaji lakini Wachezaji hao wanapatikana? Upo umuhimu lakini
Wachezaji tunaowataka hawapatikani Mwezi Januari.”
Man United bado hawajafungua Kipengele
cha kuwaongezea Mikataba ya Mwaka mmoja mmoja ya Rio Ferdinand na
Patrice Evra, ambao Mikataba yao inamalizika mwishoni mwa Msimu na pia
hawajazungumza na Nemanja Vidic na Fabio ambao Mwezi huu, Kisheria, wako
huru kuongea na Klabu nyingine kama wakitaka kuhama.
Lakini duru za ndani ya Man United
zimedai mazungumzo na Wachezaji hao wote, pamoja na Wayne Rooney,
yatafanyika na hakuna sababu ya kuwa na mchecheto.
Vile vile imefamika zipo Klabu 6
zinamtaka Wilfried Zaha kwa Mkopo Mwezi huu Januari na ingawa Moyes
amekiri kuwa Zaha anahitaji kucheza Mechi zaidi ambazo atazipata akienda
kwingine kwa Mkopo bado hawajaamua hilo kwa vile Winga Nani ni
majeruhi.
0 comments:
Post a Comment