Monday, 27 January 2014

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WANAOHARIBU MAZINGIRA KWA KUCHIMBA MCHANGA


index
Na Maelezo Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi  ya imesema itachukua hatua za kisheria kwa wananchi wanaovamia na kuchimba mchanga katika eneo la makaburi ya Mwanakwerekwe.
Hayo yameelezwa leo huko katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani na Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Haji Omar Kheri alipokuwa akijibu suala la Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni aliyetaka kujua hatua  zinazotumika kwa wale wanaoendelea kuchimba mchanga katika eneo la makaburi Mwanakwerekwe.
Amesema sio vizuri wananchi kuendelea kuchimba mchanga katika eneo hilo la makaburi kwani kufanya hivyo ni kitendo cha kikatili  na hatua kali za kisheria zitachukiwa kwa yeyote atakaekamatwa anafanya  hivyo.
“Nawasihi sana wananchi katika kufanya vitendo hivi kuwa jambo hili sio zuri watafakari, kuwafanyia hivyo marehemu ni tendo ovu haistahiki ni kitendo cha kinyama dini zote zinakataza kufanya hivyo”, alieleza.
Aidha amesema Serikali inafahamu kuwa wananchi wanachimba mchanga katika eneo hilo hivyo itafanya juhudi kubwa za kuwadhibiti  wale wote wataokamatwa na vitendo hivyo.
Waziri Kheir amefafanua kuwa Wizara yake inaendelea kuwashajihisha wananchi pamoja na kuandaa utaratibu wa kutoa michango ili kuweza kuhifadhi eneo hilo lisiendelee kuvamiwa
Hata hivyo alisema Serikali imepanga kulitumia eneo la Kama, lililozikiwa watu waliofariki katika ajali ya MV. SPICE ISLANDERS, kuwa ni sehemu mpya ya kuzikia waislamu  ili kuondosha usumbufu.
Aidha amefahamisha kuwa eneo la makaburi la Mwanakwerekwe limekuwa dogo kutokana na kubadilika kwa matumizi ya ardhi ambapo eneo hilo lilikuwa na ukubwa wa hekta 80 za mraba na  zimebaki hekta 25 kutokana na matumizi mengine ya ardhi.

0 comments: