Saturday, 11 January 2014

RIO FERDINAND AONGOZA MASTAA WALIOTOZWA MAMILIONI,KWA KOSA LA KUTUMIA TWITTER NA FACEBOOK

 
 
LONDON, ENGLAND
FACEBOOK, WhatsApp, Instagram na Twitter, ndiyo mitandao inayotawala kwenye simu za viganjani za watumiaji wengi wa huduma hiyo kwa sasa duniani, ukiweka kando mitandao mingine ya kijamii kama Circle, Viber, Skype, Tango mingineyo.
Kwa watumiaji wa kawaida, hii ni burudani kubwa sana kwao. Lakini jambo hilo limewaingiza kwenye gharama kubwa wanasoka maarufu kwenye Ligi Kuu England kwa sababu wamewekewa mipaka ya matumizi ya mitandao hiyo ya kijamii.
Kiungo Mghana, Emmanuel Frimpong, anayekipiga kwenye kikosi cha Arsenal amejiweka kwenye hatari ya kukumbana na adhabu kali baada ya kutuma picha kwenye Instagram inayomdhihaki kocha wa Manchester United, David Moyes baada ya kufungwa na Sunderland kwenye nusu fainali ya Kombe la Ligi.
Kwenye picha hiyo, Frimpong amemwonyesha Moyes kuwa maisha ya Old Trafford yamemshinda na kuamua kurudi Goodison Park, ambapo kocha huyo anaonekana akiwa ameshika ubao ulioandikwa ‘Goodison Park’ maskani ya klabu yake ya zamani, Everton, aliyokuwa akiinoa.
Hata hivyo, Frimpong, alichukua muda mfupi sana kuiondoa picha hiyo kwenye ukurasa wake baada ya kugundua kwamba itamsababishia hasara kubwa ya kupigwa faini na klabu yake ya Arsenal, Ligi Kuu England pamoja na Chama cha Soka cha England (FA).
Matumizi ya mitandao ya kijamii kama Facebook na Twitter imewawatia hasara mastaa wengi kwenye Ligi Kuu England kutokana na kutozwa faini kali za pesa, huku baadhi wakiingia kwenye matatizo zaidi kwa kutozwa hadi Pauni 2,000 kwa kila neno waliloandika.
Staa Michael Chopra alipigwa faini ya Pauni 15,000 na klabu yake ya Blackpool baada ya kuandika ujumbe kwenye Twitter ulioponda programu za mazoezi za klabu hiyo.
Lakini, Chopra hakuwa mchezaji wa kwanza kupoteza pesa kutokana na matumizi ya Twitter, kwenye orodha hiyo baadhi yao wamo wachezaji wenye hadhi kubwa kwenye Ligi Kuu England; Ashley Cole, Rio Ferdinand na Darren Bent. Makala hii inazungumzia wanasoka nyota ambao walipoteza mamilioni ya pesa kutokana na matumizi ya mitandao ya kijamii ya  Facebook na Twitter.
Chopra apunwa Pauni 15,000
Straika huyo akiwa hajafunga bao lolote tangu alipojiunga na Blackpool kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea Ipswich mwaka jana, amejikuta kwenye matatizo baada ya kutuma ujumbe kwenye Twitter unaokosoa vifaa vya mazoezi vya timu hiyo na kudai kwamba kuna wachezaji sita tu walio makini kikosini.
Kitendo hicho kimeikera klabu hiyo kwa sababu ameonyesha dharau kubwa na hivyo kumpiga faini ya pesa hizo ambazo si kiwango kidogo kwake.

Related Posts:

0 comments: