Wednesday, 22 January 2014

RAIS WA BARCA KWA JAJI MAHAKAMANI KUHUSU UHAMISHO WA NEYMAR!


>>USIRI ULIGUBIKA UHAMISHO TOKA SANTOS!
>>MWANACHAMA BARCA AIBURUZA KLABU MAHAKAMANI IFUNGUKE!
NEYMAR_IN_BARCAJAJI wa Mahakama huko Spain amekubali kusikiliza Madai dhidi ya Rais wa Barcelona Sandro Rosell kuhusu Gharama halisi za Uhamisho wa Neymar kutoka Santos ya Brazil.
Mwezi Juni Mwaka Jana, Neymar alitambulishwa kama Mchezaji mpya wa Barca kwa Uhamisho wa Dau la Euro Milioni 57.1 lakini kuwepo kwa Makubaliano ya kuweka Vipengele vya Uhamisho huo kuwa siri vilizuia kutangazwa kwa kila kitu kuhusu biashara iliyofanyika.
Sasa Jaji huyo atasikiliza Kesi ya awali ili kuamua kama kulikuwepo na ukiukwaji wa Sheria kufuatia Malalamiko ya Mwanachama wa Barca, Jordi Cases.
Waendesha Mashitaka wa Spain wamekubaliana na Madai ya Mwanachama huyo wa Barca kwamba kulikuwepo na ukiukwaji wa Sheria kwa kutumia Mkataba Feki.
Pia, wametaja Kitita cha Euro Milioni 40 kilicholipwa kwa Kampuni ya Baba yake Neymar ambacho hakikutangazwa katika Uhamisho huo.
Juzi Jumatatu, Gazeti maarufu huko Spain, El Mundo, lilitoboa kuwa Dau halisi la kumnunua Neymar ni Euro Milioni 95 kitu ambacho kilimfanya Rais Sandro Rosell atake nafasi Mahakamani ili atoe ushahidi na kujisafisha.
Hiyo Jumatatu, Rosell, akiongea na Wanahabari alitamka: “Kuna vitu viwili nataka kusema. Kwanza Neymar aligharimu Euro Milioni 57.1. Na hili nimesema mara nyingi. La pili, ni ombi, kwa heshima namuomba Jaji aniite ili nitoe ushahidi na kumwambia kila kitu anachotaka kujua kwa sababu hamna cha kuficha!”
Katika kuisikiliza Kesi hii, Jaji Pablo Ruz anatarajiwa kukusanya taarifa toka kwa Neymar, Santos na Barcelona kabla hajamwita Rosell aende mwenyewe Mahakamani kutoa Ushahidi.

0 comments: