Thursday, 16 January 2014

MWANAMKE AMCHINJA MTOTO WAKE KAMA KUKU AKAMATWA NA POLISI

.
Mmoja kati ya  watoto  waliofanyiwa ukatili wa  kinyama (picha na maktaba yetu)
..........................................
HABARI HII IMENUKURI WA KUTOKA KWA FRANCIS GODWIN NA DIANA BISANGAO WA MATUKIO DAIMA.COM, IRINGA 
 JESHI la polisi mkoani Iringa linamshikilia mwanamke  mmoja mkazi wa Iramba kata ya Itundula wilaya ya Mufindi  kwa kumchinja shingo mtoto wake na kumtupa chooni 
Akizungumza na mtandao huu w kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhan Mungi  alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Kamanda Mungi  alimtaja mwanamke huyo kwa jina la Restuta Mdemu ambae  umri wake  haujafahamika alijifungua mtoto mwenye jinsia ya kiume muda  kabla ya  kumuua kinyama kwa kumchinja shingo yake na kumtupa chooni .
Aidha alisema kuwa mwanamke huyo  alimuua mtoto wake kwa kumchinja shingoni na kitu chenye ncha kali kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe .
Chanzo cha tukio hilo la mauaji ya kinyama kwa mtoto huyo bado hakijafahamika.

Related Posts:

0 comments: