Thursday, 9 January 2014

MKE MJAMZITO AUWAWA KWA KUMCHARAZA FIMBO TUMBUNI KISA WIVU WA MAPENZI

UKATILI ULIOPITILIZA ,AUA MKE MJAMZITO KWA KUMCHARAZA FIMBO TUMBUNI KISA WIVU WA MAPENZI 


Mama Mjamzito mfano  wa aliyeuwawa 
RPC Mungi
AMA  kweli wivu ni kidonda    mwanaume mmoja mkazi wa  kijiji   kijiji  cha  Imalutwa kata ya  Lugalo  tarafa ya  Mazome   wilaya ya Kilolo mkoani Iringa kuua mkewe  mjamzito  kwa  kumcharaza fimbo hadi  kifo kwa  wivu wa kimapenzi .

Imedaiwa  kuwa  mwanaume  huyo Vicent Kasenegala (40) aliingiwa na  wivu wa  kimapenzi  na  kuamua kuanza kumcharaza  fimbo  za  tumbo mkewe  kufuatia tabia  ya  mwanamke  huyo  kuhisiwa  kuwa na mahusiano  ya kimapenzi na rafiki  zake wa karibu.

Hivyo  kutokana na hisia hizo Kasenegala aliamua  kuchukua uamuzi wa kutoa adhabu kali kwa  mkewe kwa  kuanza  kumcharaza  fimbo  katika maeneo mbali mbali ya  mwili  wake zikiwemo  fimbo  za  tumbo .

Kamanda  wa   polisi  wa  mkoa  wa Iringa  Ramadhan Mungi aliuthibitishia mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kutokea  tukio hilo  leo   wakati akizungumza na mtandao huu wa www.matukiodaima.com   ofisini  kwake na  kuwa tukio hilo  lilitokea  January 7 majira ya saa 10 jioni mwaka  huu katika  kitongoji cha Malawi  kijiji   cha Imalutwa .

Hata  hivyo  alisema  kuwa  mtuhumiwa   huyo Bw Kasenegala anatuhumiwa  kumuua mkewe  Laurencia Chusi (33) ambae alikuwa akijishughulisha na  shughuli za  kilimo  na  baada ya  tukio hilo mtuhumiwa huyo akitoweka  kusiko julikana na jeshi  la polisi bado  linaendelea  kumsaka  kwa  tuhuma  za mauwaji .
 

Related Posts:

0 comments: