Wednesday, 8 January 2014

MAPINDUZI CUP-MIAKA 50: NUSU FAINALI, SAFU YATIMIA BONGO v UGANDA!!

>>NUSU FAINALI NI BONGO v UGANDA!!
Mapinduzi Cup, Kombe la Kusheherekea Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Usiku huu limemaliza Mechi zakeZANZIBAR_STONE_TOWN za Robo Fainali na Mechi za Nusu Fainali zitashindaniwa na Timu toka Uganda dhidi ya Timu kutoka Tanzania Bara katika Mechi zote mbili.
Mabigwa Watetezi, Azam FC, wao walitinga Nusu Fainali kwa kuichapa Clove Stars, Kombaini ya Pemba, Bao 2-0, URA ya Uganda kuitungua KMKM 1-0, Tusker ya Kenya na KCC ya Uganda kutoka 0-0 katika Dakika 90 na KCC kuibuka Mshindi kwa Mikwaju ya Penati.
Simba, wakicheza Mechi ya mwisho ya Robo Fainali Uwanjani Amaan Saa mbili Usiku huu waliichapa Chuoni ya Zanzibar Bao 2-0, Bao zote zikifungwa na Ramadhan Singano.

RATIBA/MATOKEO:
ROBO FAINALI
Jumatano Januari 8
Gombani Stadium, Pemba
KMKM 0 URA 1
Azam FC 2 Clove Stars 0
Amaan Stadium
Tusker 0 KCC 0 [KCC imesonga kwa Penati 4-3]
Simba 2 Chuoni 0
NUSU FAINALI
Ijumaa Januari 10
SAA 10 JIONI: Azam FC v KCC
SAA 2 USIKU: URA v Simba

Nusu Fainali, ambazo zitachezwa Ijuma Januari 10, Azam FC itaivaa KCC na Simba kupambana na URA.
Fainali ni Jumatatu Januari 13 kwenye Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.

0 comments: