>>FUNGUA DIMBA JUMAMOSI: HULL v CHELSEA!
>>FUNGA DIMBA JUMAMOSI: MAN UNITED v SWANSEA!
SOMA ZAIDI:
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi Januari 11
[Saa za Bongo]
1545 Hull v Chelsea
1800 Cardiff v West Ham
1800 Everton v Norwich
1800 Fulham v Sunderland
1800 Southampton v West Brom
1800 Tottenham v Crystal Palace
2030 Man United v Swansea
+++++++++++++++++++++++
HULL CITY v CHELSEA
-KC Stadium
Hull City wameshinda Mechi moja tu ya
Ligi katika 7 na hiyo ni kipondo cha Bao 6-0 walipoitwanga Fulham na
wanakutana na Chelsea ambayo Magoli yao hufungwa na Viungo, si
Mastraika, huku Oscar, Eden Hazard na Willian, wakiwa hatari ingawa
watamkosa Majeruhi Frank Lampard ambae ni Kiungo wao Veterani na mahiri
kwa Mabao.
CARDIFF CITY v WEST HAM UNITED
-Cardiff City Stadium
Hii ni Mechi ya kwanza ya Ligi kwa
Lejendari wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer, tangu atwae
Umeneja wa Cardiff City Wiki iliyopita ambapo katika Mechi yake ya
kwanza kabisa waliifunga Newcastle 2-0 kwenye FA CUP.
Cardiff wanakutana na West Ham ambayo
iko mashakani kwa kushinda Mechi moja tu katika 10 na katika Mechi zao
mbili zilizopita walibandikwa 5-0 na Nottingham Forest kwenye FA CUP na
kuwashwa 6-0 na Man City kwenye Capital One Cup.
Balaa zaidi kwao ni kuwa wanatinga Mechi hii bila Nahodha wao mzoefu Kevin Nolan ambae yuko Kifungoni kwa Kadi Nyekundu.
EVERTON V NORWICH CITY
-Goodison Park
Norwich hawajashinda katika Mechi 5 za Ligi lakini hawatafurahia kukutana na Everton ingawa Everton haijawafunga tangu 2005.
FULHAM V SUNDERLAND
-Craven Cottage
Hii ni Mechi ya ‘Piga Ua’ kwani Sunderland wako mkiani na Fulham wanahitaji ushindi ili wawe Pointi 5 toka Timu 3 za mkiani.
SOUTHAMPTON V WEST BROMWITH ALBION
-St Mary’s
Timu hizi mbili zimeshinda Mechi 2 tu kati ya Mechi 19 za Ligi walizocheza Msimu huu.
West Brom watakuwa chini ya Meneja wa
muda, Keith Downing, ambae pia ni Kocha Msaidizi na ambae amewasaidia
kutofungwa katika Mechi 4 za Ligi akikaimu Nafasi hiyo, kwa mara ya
mwisho baada kuteuliwa Meneja mpya Pepe Mel kutoka Spain
TOTTENHAM V CRYSTAL PALACE
-White Hart Lane
Tangu Tim Sherwood achukue Umeneja na
kumrudisha Uwanjani Emmanuel Adebayor, Tottenham wamekuwa moto kwa
kunyakua Pointi 10 katika Mechi za Ligi 4 huku Adebayor akipiga Bao 3.
Katika Mechi ya kwanza ya Ligi Msimu huu, Penati ya Roberto Soldado iliwapa ushindi Tottenham dhidi ya Cardiff.
MANCHESTER UNITED V SWANSEA CITY
-Old Trafford
Hii ni mara ya pili kwa Man United kukutana na Swansea City Uwanjani Old Trafford ndani ya Siku 6.
Swansea walishinda kwa mara ya kwanza
kabisa walipoifunga Man United 2-1 kwenye Kombe la FA Jumapili iliyopita
lakini pengine Meneja wa Swansea, Michael Laudrup, angependelea Pointi
zaidi baada ya kutoshinda katika Mechi 6 za Ligi zilizopita.
Lakini wanakutana na Man United ambayo
haijashinda Mechi yeyote kwa Mwaka 2014 baada kuchapwa Mechi zao zote 3
Mwaka huu na ambao wanatarajiwa kuingia na moto mkali.
NEWCASTLE UNITED V MANCHESTER CITY
-St James’ Park
Tangu Manuel Pellegrini atue Manchester
City ndio kwanza wameshinda Mechi mbili za Ugenini hivi Juzi na
inaelekea wanaweza kushinda Mechi hii kwa vile Newcastle hawajaifunga
City tangu 2005.
STOKE CITY V LIVERPOOL
-Britannia Stadium
Liverpool wanaweza kuimarika kwa kurudi
kilingeni kwa Straika Daniel Sturridge lakini wana tatizo kubwa la Mechi
za Ugenini ambapo wameambua Pointi 4 tu kati Mechi zao 6 zilizopita.
Stoke, ambao walifungwa kwa Bao la
Sturridge huko Anfield Mwezi Agosti, hawajafungwa katika Mechi 7 za Ligi
za Nyumbani na hawajafungwa na Liverpool wakiwa kwao Britannia kwenye
Ligi Kuu kwa kushinda Mechi 3 na Sare 2.
ASTON VILLA V ARSENAL
-Villa Park
Hii ni nafasi murua kwa Arsene Wenger
kulipiza kisasi kwa kubamizwa Bao 3-1 kwao Emirates Siku ya ufunguzi wa
Msimu mpya wa Ligi Mwezi Agosti.
Straika wa Aston Villa Christian Benteke
alipiga Bao 2 katika kipigo hicho cha 3-1 lakini hajafunga Bao katika
Mechi 12 za Ligi na hili linachangia Villa kufunga Bao 7 tu katika Mechi
zao 10 za Nyumbani.
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumapili Januari 12
1705 Newcastle v Man City
1910 Stoke v Liverpool
Jumatatu Januari 13
2300 Aston Villa v Arsenal
MSIMAMO:
NA |
TIMU |
P |
GD |
PTS |
1 |
Arsenal |
20 |
21 |
45 |
2 |
Man City |
20 |
34 |
44 |
3 |
Chelsea |
20 |
19 |
43 |
4 |
Liverpool |
20 |
23 |
39 |
5 |
Everton |
20 |
13 |
38 |
6 |
Tottenham |
20 |
-1 |
37 |
7 |
Man Utd |
20 |
9 |
34 |
8 |
Newcastle |
20 |
4 |
33 |
9 |
Southampton |
20 |
3 |
27 |
10 |
Hull |
20 |
-3 |
23 |
11 |
Aston Villa |
20 |
-6 |
23 |
12 |
Stoke |
20 |
-11 |
22 |
13 |
Swansea |
20 |
-2 |
21 |
14 |
West Brom |
20 |
-4 |
21 |
15 |
Norwich |
20 |
-16 |
20 |
16 |
Fulham |
20 |
-21 |
19 |
17 |
Cardiff |
20 |
-17 |
18 |
18 |
Crystal Palace |
20 |
-16 |
17 |
19 |
West Ham |
20 |
-11 |
15 |
20 |
Sunderland |
20 |
-18 |
14 |
0 comments:
Post a Comment