Friday, 17 January 2014

ANGALIA NGUMI ZILIVYO PIGWA KATIKA BONGE LA UKRAINE KWA MARA NYINGINE TENA

wabunge mashati
Picha ya ajabu inaonyesha wabunge wakishikana mashati wakati wa mjadala huo na wa bajeti ya serikali.
.Bingwa wa zamani wa masumbwi uzito wa juu duniani ashuhudia ngumi zikipigwa kati ya wabunge
.Ni Vitaly Klitschko, wengi wakaa mbali naye kwenye malumbano ndani ya ukumbi wa bunge huko Kiev 
Na Damas Makangale, MOblog kwa Msaada wa Mtandao
WAKATI huku nyumbani Tanzania, viongozi wa bunge wamezoea kuita askari wa bunge kwa msaada wa kuwatoa baadhi ya wabunge wenye misimamo tofauti na kiti, huko kwa wenzetu ni ngumi tu kupigwa kama wabunge hawaelewani katika miswada mbalimbali inayojadiliwa bungeni.
Hayo yametokea tena nchini Ukraine baada ya wabunge wa bunge la nchi hiyo kuamua kuzichapa kavu kavu kwa kutumia ngumi, vichwa na mateke na kupelekea mmoja wa watunga sheria hao kupasuka kati kati ya paji la uso.
mbunge damu
Demokrasia ina njia mbalimbali za kuonyesha yenyewe …
Katika nchi ya Uingereza bunge lao kubwa la Westminster, ambalo ni mama wa mabunge yote mawili wanatumia njia ya kama kuzomea “yay au baaaa” kushawishi au kupinga hoja.
Lakini katika nchi ya Ukraine ni vigumu spika au naibu spika na wabunge wenyewe kukwepa makonde ni jambo lililozoeleka wakati wowote panapokuwa na tofauti juu ya upigaji kura katika miswada mbalimbali.
Lakini wabunge hao wakipambana wana hakikisha wanakuwa mbali na mbunge mwenzao ambaye ni bingwa wa zamani wa uzito wa juu Vitaly Klitscho ambaye kwa hakika akitaka kuzipiga kavu kavu watapasuka wengi duru za siasa zinasema kutoka katika jiji la Kiev.
Wachambuzi wa mambo na hasa siasa za Kiev wanasema kwamba si mara ya kwamza kwa viongozi wa Ukraine kuzichapa kavu kavu ndani ya ukumbi wa bunge wengine wanadiriki kusema ni utamaduni wao.
damu mbunge
Mmoja ya mbunge akibubunjika damu.
Vitali Klitschko kiongozi wa chama UDAR chenye ushawishi mkubwa ndani ya ukumbi wa bunge.
Tofauti ziliibuka pale serikali kwa mshangao wa wapinzani ilipokuja na muswada wa sheria kali za kupiga marufuku maandamano ya mitaani baada ya kuingia mikataba kadhaa ya biashara na umoja wa ulaya (EU).
Kambi ya upinzania bungeni ilikataa kata kata na muswada huo na ndipo machafuko yalipoanza na baadhi ya mawaziri na wabunge wa chama kinachotawala kuchapwa mako

Related Posts:

0 comments: