Wednesday, 12 February 2014

SERIKALI MOJA, MBILI AU TATU TUMWAMINI NANI,JAJI WARIOBA AU MWANASIASA?


Ndugu zangu,
Kwa akili ya kawaida kabisa, mwanadamu unaweza kupata tabu kuamini kuwa TUME ile ya Warioba iliyoundwa na wateule wa Rais wakiwemo wasomi mahiri, majaji na maprofesa, ikatoka na mapendekezo ya Kijinga-jinga kama hili la Muundo wa Serikali Tatu kama wengine wanavyotaka tuamini.
Nimepata kusema, kuwa haiyumkini Majaji wetu hawa wazaliwa na wazalendo wa nchi hii wakawa wote wana matatizo katika kufikiri kwao; Jaji Francis Nyalali, Jaji Robert Kissanga, Jaji Joseph Warioba, Jaji Augustine Ramadhan na Jaji Mark Bomani. Kwamba wote hawa, na katika nyakati tofauti, wamependekeza mfumo wa Serikali Tatu ili kuunusuru na kuuimarisha Muungano wetu.
Nahofia, kuwa baadhi ya wanasiasa wetu ndio wenye matatizo katika kufikiri kwao, na pengine wana ' Intellectual arrogance'- Ujivuni wa kiakili.
Na isije ikawa, kuwa wanaangalia kwanza ni mfumo gani wa Serikali utakaowanufaisha wao binafsi, makundi yao na vyama vyao kwa kuangalia namna watavyoshinda chaguzi za kisiasa na kushika madaraka.
Wanaangalia zaidi leo na kesho. Kwao kesho kutwa na mtondogoo ni mbali sana.
Naam, tumwamini nani? Maana, iliimbwa, kuwa ' Mwanasiasa' ni ' kigeugeu! Na Jaji naye....?
Habari hii imendikwa na Maggid Mjengwa,
Bagamoyo.
0754 678 252

Related Posts:

0 comments: