Tuesday, 11 February 2014

RONALDO AIPELEKA REAL MADRID FAINALI ZA KOMBE LA COPA DEL REY

ronaaldo_7ed00.jpg
Christiano Ronaldo jana aliiwezesha timu yake ya Real Madrid kutinga katika fainali za kombe la Copa Del Rey baada ya kuichapa Atletico Madrid katika mtanange wa Madrid derby; ushindi huo wa magoli 2-0 tayari umeipa timu ya Real Madrid jumla ya magoli 5-0 dhidi ya maadui zao hao wakubwa (Atletico Madrid) kwa kuwa katika mchezo ulioshuhudiwa jumaatano ya wiki iliyopita wakati Real Madrid ilipoitandika Atletico magoli 3-0 katika uwanja wa Sentiago Bernabeu.
Real Madrid sasa inamsubiri mshindi kati ya Barcelona au Real Sociedad ili kukutana katika mchezo wa fainali za kombe hilo zitakazichezwa mwezi Marchi; ikumbukwe kuwa timu ya Barcelona iliifunga timu ya Real Sociedad magoli 2-0 ikiwa katika uwanja wake wa nyumbani na timu hizo tinakutana tena leo katika mzunguko wa pili wa kombe hilo la Copa Del Rey.
Chanzo, goal.com

Related Posts:

0 comments: