Thursday, 13 February 2014

POLISI IRINGA WAMWACHIA MWENYEKITI WA WAANDISHI WA HABARI BAADA YA KUKOSA UKWELI


Wanahabari  Iringa  wakiwa na mwenyekiti wao aliyeachiwa  huru Frank Leonard wa  nne kushoto baada ya kuachiwa  huru na jeshi la polisi  leo
........................................................................
Askari  wa  jeshi la polisi mkoa  wa  Iringa  wamemwachia huru  mwenyekiti  wa chama cha  waandishi  wa  habari  mkoa  wa  Iringa (IPC) Frank Leonard ambae ni mwandishi wa magazeti ya  serikali mkoani Iringa aliyekamatwa ndani ya  chumba  cha mahakama  wakati akifuatilia mwenendo wa  kesi ya mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwenyekiti wa IPC Marehemu  Daudi Mwangosi.


Polisi hao  wamemwachia  huru  Leonard  baada ya  kukosa  ukweli  wa  kesi  hiyo  waliyotaka kumbambikia  kuwa  amepiga picha mahakamani wakati mtuhumiwa  wa mauwaji hayo ambae ni askari mwenzao akisomewa mashtaka yake.


Hata  hivyo mwanahabari huyo ambae  hakuwa amewasha kamera yake mahakamani hapo  alikuwa ameshika simu yake kabla ya askatri mmoja  kusimama na kumkamata ndani ya mahakama  wakati  kesi hiyo ikiendelea.

Related Posts:

0 comments: