Wananchi wa Kijiji cha Ndulamo Makete kilichokumbwa na janga la kuezuliwa Nyumba chapata muafaka wa hatma ya Nyumba zao
Na Edwin Moshi, Makete
Kufuatia
kijiji cha Ndulamo wilaya ya Makete mkoani Njombe kukumbwa na janga la
upepo mkali na kuezua nyumba 10 pamoja na jiko la shule ya msingi
Ndulamo Jumamosi Februari 15, mkuu wa wilaya ya Makete kwa kushirikiana
na viongozi mbalimbali na wananchi wamefanya mkutano wa hadhara kijijini
hapo kupata ufumbuzi wa janga hilo.
Mkutano
huo uliofanyika leo kijijini hapo umewahusisha wananchi wote wa kijiji
hicho ambao wamejitoa kwa hali na mali kuhakikisha janga hilo
lililokikumba kijiji hicho linattuliwa kwa pamoja.
Akiongea
kwenye mkutano huo Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro amesema
janga hilo haliwezi kutatuliwa na serikali pekee bali ushirikiano wa
pamoja baina ya serikali na wananchi ukiunganishwa pamoja utasaidia
kuwasaidia wananchi wote waliopatwa na janga hilo.
Amesema
kwa taarifa zilizopatikana kutokana na janga hilo zinaonesha kuwa
nyumba 10 pamoja na jiko la shule ya msingi Ndulamo zilizokuwa
zinakaliwa na kaya 8 zenye watu 34 ziliezuliwa pamoja na baadhi ya miti
ya mbao na ya kuni iliyokuwa jirani na kitongoji cha kwa yuta
kilichoathirika zaidi
Matiro
amesema kamati ya ulinzi na usalama ilitembelea eneo lililopata janga
hilo Februari 16, na kujionea athari zilizotokea ambapo walilazimika
kuitisha mkutano wa hadhara uliofanyika hii leo
Mkazi
wa kijiji hicho Juma Mahenge akizungumza kwenye kikao hicho amesema wao
kama wananchi wameguswa na janga hilo na kupendekeza ipitishwe harambee
kila mwananchi aliyehudhuria kutoa mchango wake na kitakachopatikana
kielekezwe kwa wahanga.
“Mimi
napendekeza wananchi tutoe kila tulicho nacho, iwe fedha, mbao,
matofali, na pia kijiji hiki kina mafundi basi tuwaombe wajitolee
kujenga nyumba hizo bure ama kama watahitaji fedha kidogo basi michango
hii itumike kuwalipa mafundi hao” alisema Mahenge
Katika
mkutano huo wamekubaliana kila kitongoji cha kijiji hicho kichangie
ujenzi wa nyumba zilizobomoka na kila kijiji kimepewa nyumba za
kuzihudumia, Msitu wa kijiji pamoja na miti iliyoanguka ipasuliwe mbao
kwa ajili ya waathirika, na mafundi walioko kijijini hapo wasaidie
katika ujenzi wa nyumba zilizobomoka ambapo kila fundi alikabidhiwa
nyumba ya kujenga
Aidha
ilifanyika harambee kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo ambapo jumla ya
sh. 940,000/= zilipatikana katika harambee hiyo, na pia mfuko wa jimbo
utasaidia kununua mabti kwa wathirika, ikisaidiwa na mchango kutoka
ofisi ya mkuu wa wilaya na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri
Wakati
huu ambapo jitihada zikiendelea wananchi waliopatwa na janga hili
wanahifadhiwa na ndugu na jamaa katika kijiji cha Ndulamo, na mkuu wa
wilaya amesema kuwa wanatarajia ndani ya wiki mbili wananchi hao
watakuwa wameshapata makazi yao.
0 comments:
Post a Comment